< Psalmorum 81 >
1 In finem, pro torcularibus. Psalmus ipsi Asaph. Exsultate Deo adjutori nostro; jubilate Deo Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Sumite psalmum, et date tympanum; psalterium jucundum cum cithara.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Buccinate in neomenia tuba, in insigni die solemnitatis vestræ:
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 quia præceptum in Israël est, et judicium Deo Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 Testimonium in Joseph posuit illud, cum exiret de terra Ægypti; linguam quam non noverat, audivit.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 Divertit ab oneribus dorsum ejus; manus ejus in cophino servierunt.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 In tribulatione invocasti me, et liberavi te. Exaudivi te in abscondito tempestatis; probavi te apud aquam contradictionis.
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Audi, populus meus, et contestabor te. Israël, si audieris me,
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 non erit in te deus recens, neque adorabis deum alienum.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 Ego enim sum Dominus Deus tuus, qui eduxi te de terra Ægypti. Dilata os tuum, et implebo illud.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 Et non audivit populus meus vocem meam, et Israël non intendit mihi.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 Et dimisi eos secundum desideria cordis eorum; ibunt in adinventionibus suis.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Si populus meus audisset me, Israël si in viis meis ambulasset,
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 pro nihilo forsitan inimicos eorum humiliassem, et super tribulantes eos misissem manum meam.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 Inimici Domini mentiti sunt ei, et erit tempus eorum in sæcula.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 Et cibavit eos ex adipe frumenti, et de petra melle saturavit eos.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”