< Psalmorum 75 >
1 In finem, ne corrumpas. Psalmus cantici Asaph. Confitebimur tibi, Deus, confitebimur, et invocabimus nomen tuum; narrabimus mirabilia tua.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Cum accepero tempus, ego justitias judicabo.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Liquefacta est terra et omnes qui habitant in ea: ego confirmavi columnas ejus.
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Dixi iniquis: Nolite inique agere: et delinquentibus: Nolite exaltare cornu:
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 nolite extollere in altum cornu vestrum; nolite loqui adversus Deum iniquitatem.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 Quia neque ab oriente, neque ab occidente, neque a desertis montibus:
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 quoniam Deus judex est. Hunc humiliat, et hunc exaltat:
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 quia calix in manu Domini vini meri, plenus misto. Et inclinavit ex hoc in hoc; verumtamen fæx ejus non est exinanita: bibent omnes peccatores terræ.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Ego autem annuntiabo in sæculum; cantabo Deo Jacob:
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 et omnia cornua peccatorum confringam, et exaltabuntur cornua justi.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.