< Psalmorum 30 >

1 Psalmus cantici, in dedicatione domus David. Exaltabo te, Domine, quoniam suscepisti me, nec delectasti inimicos meos super me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Domine Deus meus, clamavi ad te, et sanasti me.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Domine, eduxisti ab inferno animam meam; salvasti me a descendentibus in lacum. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Psallite Domino, sancti ejus; et confitemini memoriæ sanctitatis ejus.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 Quoniam ira in indignatione ejus, et vita in voluntate ejus: ad vesperum demorabitur fletus, et ad matutinum lætitia.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Ego autem dixi in abundantia mea: Non movebor in æternum.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Domine, in voluntate tua præstitisti decori meo virtutem; avertisti faciem tuam a me, et factus sum conturbatus.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Ad te, Domine, clamabo, et ad Deum meum deprecabor.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 Quæ utilitas in sanguine meo, dum descendo in corruptionem? numquid confitebitur tibi pulvis, aut annuntiabit veritatem tuam?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Audivit Dominus, et misertus est mei; Dominus factus est adjutor meus.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Convertisti planctum meum in gaudium mihi; conscidisti saccum meum, et circumdedisti me lætitia:
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 ut cantet tibi gloria mea, et non compungar. Domine Deus meus, in æternum confitebor tibi.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalmorum 30 >