< Psalmorum 149 >

1 Alleluja. Cantate Domino canticum novum; laus ejus in ecclesia sanctorum.
Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
2 Lætetur Israël in eo qui fecit eum, et filii Sion exsultent in rege suo.
Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
3 Laudent nomen ejus in choro; in tympano et psalterio psallant ei.
Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
4 Quia beneplacitum est Domino in populo suo, et exaltabit mansuetos in salutem.
Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
5 Exsultabunt sancti in gloria; lætabuntur in cubilibus suis.
Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
6 Exaltationes Dei in gutture eorum, et gladii ancipites in manibus eorum:
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
7 ad faciendam vindictam in nationibus, increpationes in populis;
kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
8 ad alligandos reges eorum in compedibus, et nobiles eorum in manicis ferreis;
Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
9 ut faciant in eis judicium conscriptum: gloria hæc est omnibus sanctis ejus. Alleluja.
Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.

< Psalmorum 149 >