< Psalmorum 141 >
1 Psalmus David. Domine, clamavi ad te: exaudi me; intende voci meæ, cum clamavero ad te.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 Dirigatur oratio mea sicut incensum in conspectu tuo; elevatio manuum mearum sacrificium vespertinum.
Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 Pone, Domine, custodiam ori meo, et ostium circumstantiæ labiis meis.
Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 Non declines cor meum in verba malitiæ, ad excusandas excusationes in peccatis; cum hominibus operantibus iniquitatem, et non communicabo cum electis eorum.
Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Corripiet me justus in misericordia, et increpabit me: oleum autem peccatoris non impinguet caput meum. Quoniam adhuc et oratio mea in beneplacitis eorum:
Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
6 absorpti sunt juncti petræ judices eorum. Audient verba mea, quoniam potuerunt.
watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
7 Sicut crassitudo terræ erupta est super terram, dissipata sunt ossa nostra secus infernum. (Sheol )
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol )
8 Quia ad te, Domine, Domine, oculi mei; in te speravi, non auferas animam meam.
Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9 Custodi me a laqueo quem statuerunt mihi, et a scandalis operantium iniquitatem.
Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Cadent in retiaculo ejus peccatores: singulariter sum ego, donec transeam.
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.