< Psalmorum 129 >
1 Canticum graduum. Sæpe expugnaverunt me a juventute mea, dicat nunc Israël;
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 sæpe expugnaverunt me a juventute mea: etenim non potuerunt mihi.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 Supra dorsum meum fabricaverunt peccatores; prolongaverunt iniquitatem suam.
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 Dominus justus concidit cervices peccatorum.
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Confundantur, et convertantur retrorsum omnes qui oderunt Sion.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Fiant sicut fœnum tectorum, quod priusquam evellatur exaruit:
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 de quo non implevit manum suam qui metit, et sinum suum qui manipulos colligit.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Et non dixerunt qui præteribant: Benedictio Domini super vos. Benediximus vobis in nomine Domini.
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”