< Psalmorum 111 >
1 Alleluja. Confitebor tibi, Domine, in toto corde meo, in consilio justorum, et congregatione.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 Magna opera Domini: exquisita in omnes voluntates ejus.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 Confessio et magnificentia opus ejus, et justitia ejus manet in sæculum sæculi.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 Memoriam fecit mirabilium suorum, misericors et miserator Dominus.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 Escam dedit timentibus se; memor erit in sæculum testamenti sui.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 Virtutem operum suorum annuntiabit populo suo,
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 ut det illis hæreditatem gentium. Opera manuum ejus veritas et judicium.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 Fidelia omnia mandata ejus, confirmata in sæculum sæculi, facta in veritate et æquitate.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 Redemptionem misit populo suo; mandavit in æternum testamentum suum. Sanctum et terribile nomen ejus.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 Initium sapientiæ timor Domini; intellectus bonus omnibus facientibus eum: laudatio ejus manet in sæculum sæculi.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.