< Psalmorum 111 >

1 Alleluja. Confitebor tibi, Domine, in toto corde meo, in consilio justorum, et congregatione.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Magna opera Domini: exquisita in omnes voluntates ejus.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Confessio et magnificentia opus ejus, et justitia ejus manet in sæculum sæculi.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 Memoriam fecit mirabilium suorum, misericors et miserator Dominus.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Escam dedit timentibus se; memor erit in sæculum testamenti sui.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 Virtutem operum suorum annuntiabit populo suo,
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 ut det illis hæreditatem gentium. Opera manuum ejus veritas et judicium.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 Fidelia omnia mandata ejus, confirmata in sæculum sæculi, facta in veritate et æquitate.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Redemptionem misit populo suo; mandavit in æternum testamentum suum. Sanctum et terribile nomen ejus.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Initium sapientiæ timor Domini; intellectus bonus omnibus facientibus eum: laudatio ejus manet in sæculum sæculi.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalmorum 111 >