< Proverbiorum 3 >
1 Fili mi, ne obliviscaris legis meæ, et præcepta mea cor tuum custodiat:
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 longitudinem enim dierum, et annos vitæ, et pacem, apponent tibi.
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3 Misericordia et veritas te non deserant; circumda eas gutturi tuo, et describe in tabulis cordis tui:
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4 et invenies gratiam, et disciplinam bonam, coram Deo et hominibus.
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5 Habe fiduciam in Domino ex toto corde tuo, et ne innitaris prudentiæ tuæ.
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 In omnibus viis tuis cogita illum, et ipse diriget gressus tuos.
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7 Ne sis sapiens apud temetipsum; time Deum, et recede a malo:
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8 sanitas quippe erit umbilico tuo, et irrigatio ossium tuorum.
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9 Honora Dominum de tua substantia, et de primitiis omnium frugum tuarum da ei:
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10 et implebuntur horrea tua saturitate, et vino torcularia tua redundabunt.
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11 Disciplinam Domini, fili mi, ne abjicias, nec deficias cum ab eo corriperis:
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12 quem enim diligit Dominus, corripit, et quasi pater in filio complacet sibi.
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13 Beatus homo qui invenit sapientiam, et qui affluit prudentia.
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14 Melior est acquisitio ejus negotiatione argenti, et auri primi et purissimi fructus ejus.
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15 Pretiosior est cunctis opibus, et omnia quæ desiderantur huic non valent comparari.
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16 Longitudo dierum in dextera ejus, et in sinistra illius divitiæ et gloria.
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17 Viæ ejus viæ pulchræ, et omnes semitæ illius pacificæ.
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18 Lignum vitæ est his qui apprehenderint eam, et qui tenuerit eam beatus.
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19 Dominus sapientia fundavit terram; stabilivit cælos prudentia.
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20 Sapientia illius eruperunt abyssi, et nubes rore concrescunt.
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21 Fili mi, ne effluant hæc ab oculis tuis. Custodi legem atque consilium,
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22 et erit vita animæ tuæ, et gratia faucibus tuis.
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23 Tunc ambulabis fiducialiter in via tua, et pes tuus non impinget.
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24 Si dormieris, non timebis; quiesces, et suavis erit somnus tuus.
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25 Ne paveas repentino terrore, et irruentes tibi potentias impiorum.
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26 Dominus enim erit in latere tuo, et custodiet pedem tuum, ne capiaris.
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27 Noli prohibere benefacere eum qui potest: si vales, et ipse benefac.
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28 Ne dicas amico tuo: Vade, et revertere: cras dabo tibi: cum statim possis dare.
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29 Ne moliaris amico tuo malum, cum ille in te habeat fiduciam.
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30 Ne contendas adversus hominem frustra, cum ipse tibi nihil mali fecerit.
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31 Ne æmuleris hominem injustum, nec imiteris vias ejus:
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32 quia abominatio Domini est omnis illusor, et cum simplicibus sermocinatio ejus.
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33 Egestas a Domino in domo impii; habitacula autem justorum benedicentur.
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34 Ipse deludet illusores, et mansuetis dabit gratiam.
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35 Gloriam sapientes possidebunt; stultorum exaltatio ignominia.
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.