< Job 8 >

1 Respondens autem Baldad Suhites, dixit:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 Usquequo loqueris talia, et spiritus multiplex sermones oris tui?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Numquid Deus supplantat judicium? aut Omnipotens subvertit quod justum est?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Etiam si filii tui peccaverunt ei, et dimisit eos in manu iniquitatis suæ:
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 tu tamen si diluculo consurrexeris ad Deum, et Omnipotentem fueris deprecatus;
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 si mundus et rectus incesseris: statim evigilabit ad te, et pacatum reddet habitaculum justitiæ tuæ,
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 in tantum ut si priora tua fuerint parva, et novissima tua multiplicentur nimis.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Interroga enim generationem pristinam, et diligenter investiga patrum memoriam
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 (hesterni quippe sumus, et ignoramus, quoniam sicut umbra dies nostri sunt super terram),
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 et ipsi docebunt te, loquentur tibi, et de corde suo proferent eloquia.
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Numquid vivere potest scirpus absque humore? aut crescere carectum sine aqua?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Cum adhuc sit in flore, nec carpatur manu, ante omnes herbas arescit.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Sic viæ omnium qui obliviscuntur Deum, et spes hypocritæ peribit.
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Non ei placebit vecordia sua, et sicut tela aranearum fiducia ejus.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 Innitetur super domum suam, et non stabit; fulciet eam, et non consurget.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 Humectus videtur antequam veniat sol, et in ortu suo germen ejus egredietur.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 Super acervum petrarum radices ejus densabuntur, et inter lapides commorabitur.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 Si absorbuerit eum de loco suo, negabit eum, et dicet: Non novi te.
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Hæc est enim lætitia viæ ejus, ut rursum de terra alii germinentur.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Deus non projiciet simplicem, nec porriget manum malignis,
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 donec impleatur risu os tuum, et labia tua jubilo.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Qui oderunt te induentur confusione, et tabernaculum impiorum non subsistet.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.

< Job 8 >