< Psalmorum 73 >

1 Psalmus Asaph. Quam bonus Israel Deus his, qui recto sunt corde!
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Mei autem pene moti sunt pedes: pene effusi sunt gressus mei.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Quia zelavi super iniquos, pacem peccatorum videns.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Quia non est respectus morti eorum: et firmamentum in plaga eorum.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 In labore hominum non sunt, et cum hominibus non flagellabuntur:
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Ideo tenuit eos superbia, operti sunt iniquitate et impietate sua.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Prodiit quasi ex adipe iniquitas eorum: transierunt in affectum cordis.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Cogitaverunt, et locuti sunt nequitiam: iniquitatem in excelso locuti sunt.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Posuerunt in cælum os suum: et lingua eorum transivit in terra.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Ideo convertetur populus meus hic: et dies pleni invenientur in eis.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 Et dixerunt: Quomodo scit Deus, et si est scientia in excelso?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Ecce ipsi peccatores, et abundantes in sæculo, obtinuerunt divitias.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Et dixi: Ergo sine causa iustificavi cor meum, et lavi inter innocentes manus meas:
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 Et fui flagellatus tota die, et castigatio mea in matutinis.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Si dicebam: Narrabo sic: ecce nationem filiorum tuorum reprobavi.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Existimabam ut cognoscerem hoc, labor est ante me:
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Donec intrem in Sanctuarium Dei: et intelligam in novissimis eorum.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Verumtamen propter dolos posuisti eis: deiecisti eos dum allevarentur.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Quomodo facti sunt in desolationem, subito defecerunt: perierunt propter iniquitatem suam.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Velut somnium surgentium Domine, in civitate tua imaginem ipsorum ad nihilum rediges.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Quia inflammatum est cor meum, et renes mei commutati sunt:
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 et ego ad nihilum redactus sum, et nescivi.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Ut iumentum factus sum apud te: et ego semper tecum.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Tenuisti manum dexteram meam: et in voluntate tua deduxisti me, et cum gloria suscepisti me.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Quid enim mihi est in cælo? et a te quid volui super terram?
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Defecit caro mea et cor meum: Deus cordis mei, et pars mea Deus in æternum.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Quia ecce, qui elongant se a te, peribunt: perdidisti omnes, qui fornicantur abs te.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Mihi autem adhærere Deo bonum est: ponere in Domino Deo spem meam: ut annunciem omnes prædicationes tuas, in portis filiæ Sion.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalmorum 73 >