< Psalmorum 6 >
1 In finem in carminibus, Psalmus David, pro octava. Domine, ne in furore tuo arguas me, neque in ira tua corripias me.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Miserere mei Domine quoniam infirmus sum: sana me Domine quoniam conturbata sunt ossa mea,
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 et anima mea turbata est valde: sed tu Domine usquequo?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Convertere Domine, et eripe animam meam: salvum me fac propter misericordiam tuam.
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Quoniam non est in morte qui memor sit tui: in inferno autem quis confitebitur tibi? (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 Laboravi in gemitu meo, lavabo per singulas noctes lectum meum: lacrymis meis stratum meum rigabo.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 Turbatus est a furore oculus meus: inveteravi inter omnes inimicos meos.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Discedite a me omnes qui operamini iniquitatem: quoniam exaudivit Dominus vocem fletus mei.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 Exaudivit Dominus deprecationem meam, Dominus orationem meam suscepit.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Erubescant, et conturbentur vehementer omnes inimici mei: convertantur et erubescant valde velociter.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.