< Psalmorum 120 >
1 Canticum graduum. Ad Dominum cum tribularer clamavi: et exaudivit me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Domine libera animam meam a labiis iniquis, et a lingua dolosa.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Quid detur tibi, aut quid apponatur tibi ad linguam dolosam?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Sagittæ potentis acutæ, cum carbonibus desolatoriis.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Heu mihi, quia incolatus meus prolongatus est: habitavi cum habitantibus Cedar:
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 multum incola fuit anima mea.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Cum his, qui oderunt pacem, eram pacificus: cum loquebar illis, impugnabant me gratis.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.