< Job 3 >

1 Post hæc aperuit Iob os suum, et maledixit diei suo,
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 et locutus est.
Kisha akasema:
3 Pereat dies in qua natus sum, et nox in qua dictum est: Conceptus est homo.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Dies ille vertatur in tenebras, non requirat eum Deus desuper, et non illustretur lumine.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Obscurent eum tenebræ et umbra mortis, occupet eum caligo, et involvatur amaritudine.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 Noctem illam tenebrosus turbo possideat, non computetur in diebus anni, nec numeretur in mensibus:
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Sit nox illa solitaria, nec laude digna:
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Maledicant ei qui maledicunt diei, qui parati sunt suscitare Leviathan:
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Obtenebrentur stellæ caligine eius: expectet lucem et non videat, nec ortum surgentis auroræ:
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Quia non conclusit ostia ventris, qui portavit me, nec abstulit mala ab oculis meis.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Quare non in vulva mortuus sum, egressus ex utero non statim perii?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Quare exceptus genibus? cur lactatus uberibus?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 Nunc enim dormiens silerem, et somno meo requiescerem:
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 Cum regibus et consulibus terræ, qui ædificant sibi solitudines:
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Aut cum principibus, qui possident aurum, et replent domos suas argento:
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Aut sicut abortivum absconditum non subsisterem, vel qui concepti non viderunt lucem.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 Ibi impii cessaverunt a tumultu, et ibi requieverunt fessi robore.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 Et quondam vincti pariter sine molestia, non audierunt vocem exactoris.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Parvus et magnus ibi sunt, et servus liber a domino suo.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Quare misero data est lux, et vita his, qui in amaritudine animæ sunt?
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 qui expectant mortem, et non venit, quasi effodientes thesaurum:
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Gaudentque vehementer cum invenerint sepulchrum.
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Viro cuius abscondita est via, et circumdedit eum Deus tenebris?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 Antequam comedam suspiro: et tamquam inundantes aquæ, sic rugitus meus:
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 Quia timor, quem timebam, evenit mihi: et quod verebar accidit.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 Nonne dissimulavi? nonne silui? nonne quievi? et venit super me indignatio.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >