< Job 26 >
1 Respondens autem Iob, dixit:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Cuius adiutor es? numquid imbecillis? et sustentas brachium eius, qui non est fortis?
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 Cui dedisti consilium? forsitan illi qui non habet sapientiam, et prudentiam tuam ostendisti plurimam.
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 Quem docere voluisti? nonne eum, qui fecit spiramentum?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 Ecce gigantes gemunt sub aquis, et qui habitant cum eis.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Nudus est infernus coram illo, et nullum est operimentum perditioni. (Sheol )
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol )
7 Qui extendit Aquilonem super vacuum, et appendit terram super nihilum.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Qui ligat aquas in nubibus suis, ut non erumpant pariter deorsum.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Qui tenet vultum solii sui, et expandit super illud nebulam suam.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 Terminum circumdedit aquis, usque dum finiantur lux et tenebræ.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Columnæ cæli contremiscunt, et pavent ad nutum eius.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 In fortitudine illius repente maria congregata sunt, et prudentia eius percussit superbum.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 Spiritus eius ornavit cælos: et obstetricante manu eius, eductus est coluber tortuosus.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Ecce, hæc ex parte dicta sunt viarum eius: et cum vix parvam stillam sermonis eius audierimus, quis poterit tonitruum magnitudinis illius intueri?
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”