< Genesis 11 >

1 Erat autem terra labii unius, et sermonum eorumdem.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 Cumque proficiscerentur de oriente, invenerunt campum in terra Senaar, et habitaverunt in eo.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 Dixitque alter ad proximum suum: Venite, faciamus lateres, et coquamus eos igni. Habueruntque lateres pro saxis, et bitumen pro cæmento:
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 et dixerunt: Venite, faciamus nobis civitatem et turrim, cuius culmen pertingat ad cælum: et celebremus nomen nostrum antequam dividamur in universas terras.
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 Descendit autem Dominus ut videret civitatem et turrim, quam ædificabant filii Adam,
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 et dixit: Ecce, unus est populus, et unum labium omnibus: cœperuntque hoc facere, nec desistent a cogitationibus suis, donec eas opere compleant.
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Venite igitur, descendamus, et confundamus ibi linguam eorum, ut non audiat unusquisque vocem proximi sui.
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 Atque ita divisit eos Dominus ex illo loco in universas terras, et cessaverunt ædificare civitatem.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 Et idcirco vocatum est nomen eius Babel, quia ibi confusum est labium universæ terræ: et inde dispersit eos Dominus super faciem cunctarum regionum.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 Hæ sunt generationes Sem: Sem erat centum annorum quando genuit Arphaxad, biennio post diluvium.
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 Vixitque Sem postquam genuit Arphaxad, quingentis annis: et genuit filios et filias.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 Porro Arphaxad vixit triginta quinque annis, et genuit Sale.
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 Vixitque Arphaxad postquam genuit Sale, trecentis tribus annis: et genuit filios et filias.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Sale quoque vixit triginta annis, et genuit Heber.
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Vixitque Sale postquam genuit Heber, quadringentis tribus annis: et genuit filios et filias.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 Vixit autem Heber triginta quatuor annis, et genuit Phaleg.
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Et vixit Heber postquam genuit Phaleg, quadringentis triginta annis: et genuit filios et filias.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 Vixit quoque Phaleg triginta annis, et genuit Reu.
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Vixitque Phaleg postquam genuit Reu, ducentis novem annis, et genuit filios et filias.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Vixit autem Reu triginta duobus annis, et genuit Sarug.
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 Vixit quoque Reu postquam genuit Sarug, ducentis septem annis: et genuit filios et filias.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 Vixit vero Sarug triginta annis, et genuit Nachor.
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Vixitque Sarug postquam genuit Nachor, ducentis annis: et genuit filios et filias.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 Vixit autem Nachor viginti novem annis, et genuit Thare.
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Vixitque Nachor postquam genuit Thare, centum decem et novem annis: et genuit filios et filias.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 Vixitque Thare septuaginta annis, et genuit Abram et Nachor, et Aran.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 Hæ sunt autem generationes Thare: Thare genuit Abram, Nachor, et Aran. Porro Aran genuit Lot.
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 Mortuusque est Aran ante Thare patrem suum, in terra nativitatis suæ in Ur Chaldæorum.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 Duxerunt autem Abram et Nachor uxores: nomen uxoris Abram, Sarai: et nomen uxoris Nachor, Melcha filia Aran patris Melchæ, et patris Ieschæ.
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 Erat autem Sarai sterilis, nec habebat liberos.
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 Tulit itaque Thare Abram filium suum, et Lot filium Aran, filium filii sui, et Sarai nurum suam, uxorem Abram filii sui, et eduxit eos de Ur Chaldæorum, ut irent in terram Chanaan: veneruntque usque Haran, et habitaverunt ibi.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 Et facti sunt dies Thare ducentorum quinque annorum, et mortuus est in Haran.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Genesis 11 >