< Psalmorum 92 >
1 Psalmus cantici, in die sabbati. [Bonum est confiteri Domino, et psallere nomini tuo, Altissime:
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
2 ad annuntiandum mane misericordiam tuam, et veritatem tuam per noctem,
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
3 in decachordo, psalterio; cum cantico, in cithara.
kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.
4 Quia delectasti me, Domine, in factura tua; et in operibus manuum tuarum exsultabo.
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
5 Quam magnificata sunt opera tua, Domine! nimis profundæ factæ sunt cogitationes tuæ.
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
6 Vir insipiens non cognoscet, et stultus non intelliget hæc.
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
7 Cum exorti fuerint peccatores sicut fœnum, et apparuerint omnes qui operantur iniquitatem, ut intereant in sæculum sæculi:
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
8 tu autem Altissimus in æternum, Domine.
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
9 Quoniam ecce inimici tui, Domine, quoniam ecce inimici tui peribunt; et dispergentur omnes qui operantur iniquitatem.
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
10 Et exaltabitur sicut unicornis cornu meum, et senectus mea in misericordia uberi.
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
11 Et despexit oculus meus inimicos meos, et in insurgentibus in me malignantibus audiet auris mea.
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
12 Justus ut palma florebit; sicut cedrus Libani multiplicabitur.
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
13 Plantati in domo Domini, in atriis domus Dei nostri florebunt.
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
14 Adhuc multiplicabuntur in senecta uberi, et bene patientes erunt:
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
15 ut annuntient quoniam rectus Dominus Deus noster, et non est iniquitas in eo.]
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”