< Psalmorum 78 >
1 Intellectus Asaph. [Attendite, popule meus, legem meam; inclinate aurem vestram in verba oris mei.
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Aperiam in parabolis os meum; loquar propositiones ab initio.
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Quanta audivimus, et cognovimus ea, et patres nostri narraverunt nobis.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Non sunt occultata a filiis eorum in generatione altera, narrantes laudes Domini et virtutes ejus, et mirabilia ejus quæ fecit.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Et suscitavit testimonium in Jacob, et legem posuit in Israël, quanta mandavit patribus nostris nota facere ea filiis suis:
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 ut cognoscat generatio altera: filii qui nascentur et exsurgent, et narrabunt filiis suis,
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 ut ponant in Deo spem suam, et non obliviscantur operum Dei, et mandata ejus exquirant:
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 ne fiant, sicut patres eorum, generatio prava et exasperans; generatio quæ non direxit cor suum, et non est creditus cum Deo spiritus ejus.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Filii Ephrem, intendentes et mittentes arcum, conversi sunt in die belli.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Non custodierunt testamentum Dei, et in lege ejus noluerunt ambulare.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 Et obliti sunt benefactorum ejus, et mirabilium ejus quæ ostendit eis.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Coram patribus eorum fecit mirabilia in terra Ægypti, in campo Taneos.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Interrupit mare, et perduxit eos, et statuit aquas quasi in utre:
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 et deduxit eos in nube diei, et tota nocte in illuminatione ignis.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Interrupit petram in eremo, et adaquavit eos velut in abysso multa.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 Et eduxit aquam de petra, et deduxit tamquam flumina aquas.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Et apposuerunt adhuc peccare ei; in iram excitaverunt Excelsum in inaquoso.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 Et tentaverunt Deum in cordibus suis, ut peterent escas animabus suis.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 Et male locuti sunt de Deo; dixerunt: Numquid poterit Deus parare mensam in deserto?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 quoniam percussit petram, et fluxerunt aquæ, et torrentes inundaverunt. Numquid et panem poterit dare, aut parare mensam populo suo?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Ideo audivit Dominus et distulit; et ignis accensus est in Jacob, et ira ascendit in Israël:
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 quia non crediderunt in Deo, nec speraverunt in salutari ejus.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Et mandavit nubibus desuper, et januas cæli aperuit.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 Et pluit illis manna ad manducandum, et panem cæli dedit eis.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Panem angelorum manducavit homo; cibaria misit eis in abundantia.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Transtulit austrum de cælo, et induxit in virtute sua africum.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 Et pluit super eos sicut pulverem carnes, et sicut arenam maris volatilia pennata.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 Et ceciderunt in medio castrorum eorum, circa tabernacula eorum.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Et manducaverunt, et saturati sunt nimis, et desiderium eorum attulit eis:
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 non sunt fraudati a desiderio suo. Adhuc escæ eorum erant in ore ipsorum,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 et ira Dei ascendit super eos: et occidit pingues eorum, et electos Israël impedivit.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 In omnibus his peccaverunt adhuc, et non crediderunt in mirabilibus ejus.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Et defecerunt in vanitate dies eorum, et anni eorum cum festinatione.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Cum occideret eos, quærebant eum et revertebantur, et diluculo veniebant ad eum.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 Et rememorati sunt quia Deus adjutor est eorum, et Deus excelsus redemptor eorum est.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Et dilexerunt eum in ore suo, et lingua sua mentiti sunt ei;
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 cor autem eorum non erat rectum cum eo, nec fideles habiti sunt in testamento ejus.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Ipse autem est misericors, et propitius fiet peccatis eorum, et non disperdet eos. Et abundavit ut averteret iram suam, et non accendit omnem iram suam.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Et recordatus est quia caro sunt, spiritus vadens et non rediens.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Quoties exacerbaverunt eum in deserto; in iram concitaverunt eum in inaquoso?
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Et conversi sunt, et tentaverunt Deum, et sanctum Israël exacerbaverunt.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Non sunt recordati manus ejus, die qua redemit eos de manu tribulantis:
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 sicut posuit in Ægypto signa sua, et prodigia sua in campo Taneos;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 et convertit in sanguinem flumina eorum, et imbres eorum, ne biberent.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Misit in eos cœnomyiam, et comedit eos, et ranam, et disperdidit eos;
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 et dedit ærugini fructus eorum, et labores eorum locustæ;
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 et occidit in grandine vineas eorum, et moros eorum in pruina;
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 et tradidit grandini jumenta eorum, et possessionem eorum igni;
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 misit in eos iram indignationis suæ, indignationem, et iram, et tribulationem, immissiones per angelos malos.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 Viam fecit semitæ iræ suæ: non pepercit a morte animabus eorum, et jumenta eorum in morte conclusit:
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 et percussit omne primogenitum in terra Ægypti; primitias omnis laboris eorum in tabernaculis Cham:
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 et abstulit sicut oves populum suum, et perduxit eos tamquam gregem in deserto:
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 et deduxit eos in spe, et non timuerunt, et inimicos eorum operuit mare.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Et induxit eos in montem sanctificationis suæ, montem quem acquisivit dextera ejus; et ejecit a facie eorum gentes, et sorte divisit eis terram in funiculo distributionis;
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 et habitare fecit in tabernaculis eorum tribus Israël.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Et tentaverunt, et exacerbaverunt Deum excelsum, et testimonia ejus non custodierunt.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 Et averterunt se, et non servaverunt pactum: quemadmodum patres eorum, conversi sunt in arcum pravum.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 In iram concitaverunt eum in collibus suis, et in sculptilibus suis ad æmulationem eum provocaverunt.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Audivit Deus, et sprevit, et ad nihilum redegit valde Israël.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 Et repulit tabernaculum Silo, tabernaculum suum, ubi habitavit in hominibus.
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 Et tradidit in captivitatem virtutem eorum, et pulchritudinem eorum in manus inimici.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 Et conclusit in gladio populum suum, et hæreditatem suam sprevit.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Juvenes eorum comedit ignis, et virgines eorum non sunt lamentatæ.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Sacerdotes eorum in gladio ceciderunt, et viduæ eorum non plorabantur.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Et excitatus est tamquam dormiens Dominus, tamquam potens crapulatus a vino.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 Et percussit inimicos suos in posteriora; opprobrium sempiternum dedit illis.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Et repulit tabernaculum Joseph, et tribum Ephraim non elegit:
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 sed elegit tribum Juda, montem Sion, quem dilexit.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Et ædificavit sicut unicornium sanctificium suum, in terra quam fundavit in sæcula.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Et elegit David, servum suum, et sustulit eum de gregibus ovium; de post fœtantes accepit eum:
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 pascere Jacob servum suum, et Israël hæreditatem suam.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Et pavit eos in innocentia cordis sui, et in intellectibus manuum suarum deduxit eos.]
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.