< Psalmorum 124 >
1 Canticum graduum. [Nisi quia Dominus erat in nobis, dicat nunc Israël,
“Kama Yahwe asingekuwa upande wetu,” Israeli na aseme sasa,
2 nisi quia Dominus erat in nobis: cum exsurgerent homines in nos,
“Kama asingekuwa Yahwe ambaye alikuwa upande wetu wakati watu walipoinuka dhidi yetu,
3 forte vivos deglutissent nos; cum irasceretur furor eorum in nos,
basi wangekuwa wametumeza tungali hai hasira yao lipozidi dhidi yetu.
4 forsitan aqua absorbuisset nos;
Maji yangetugharikisha; mto ungetuzidia.
5 torrentem pertransivit anima nostra; forsitan pertransisset anima nostra aquam intolerabilem.
Kisha maji yafurikayo yangetuzamisha.”
6 Benedictus Dominus, qui non dedit nos in captionem dentibus eorum.
Atukuzwe Yahwe, ambaye hajaruhusu tuwe mawindo kwa meno yao.
7 Anima nostra sicut passer erepta est de laqueo venantium; laqueus contritus est, et nos liberati sumus.
Tumetoroka kama ndege mtegoni mwa wawindaji; mtego umevunjika, nasi tumetoroka.
8 Adjutorium nostrum in nomine Domini, qui fecit cælum et terram.]
Msaada wetu uko katika Yahwe, aliyeziumba mbingu na nchi.