< Job 10 >

1 [Tædet animam meam vitæ meæ; dimittam adversum me eloquium meum: loquar in amaritudine animæ meæ.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 Dicam Deo: Noli me condemnare; indica mihi cur me ita judices.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Numquid bonum tibi videtur, si calumnieris me, et opprimas me opus manuum tuarum, et consilium impiorum adjuves?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Numquid oculi carnei tibi sunt? aut sicut videt homo, et tu videbis?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Numquid sicut dies hominis dies tui, et anni tui sicut humana sunt tempora,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 ut quæras iniquitatem meam, et peccatum meum scruteris,
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 et scias quia nihil impium fecerim, cum sit nemo qui de manu tua possit eruere?
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 Manus tuæ fecerunt me, et plasmaverunt me totum in circuitu: et sic repente præcipitas me?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Memento, quæso, quod sicut lutum feceris me, et in pulverem reduces me.
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Nonne sicut lac mulsisti me, et sicut caseum me coagulasti?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 Pelle et carnibus vestisti me; ossibus et nervis compegisti me.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 Vitam et misericordiam tribuisti mihi, et visitatio tua custodivit spiritum meum.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Licet hæc celes in corde tuo, tamen scio quia universorum memineris.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 Si peccavi, et ad horam pepercisti mihi, cur ab iniquitate mea mundum me esse non pateris?
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 Et si impius fuero, væ mihi est; et si justus, non levabo caput, saturatus afflictione et miseria.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 Et propter superbiam quasi leænam capies me, reversusque mirabiliter me crucias.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 Instauras testes tuos contra me, et multiplicas iram tuam adversum me, et pœnæ militant in me.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 Quare de vulva eduxisti me? qui utinam consumptus essem, ne oculus me videret.
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 Fuissem quasi non essem, de utero translatus ad tumulum.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Numquid non paucitas dierum meorum finietur brevi? dimitte ergo me, ut plangam paululum dolorem meum,
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 antequam vadam, et non revertar, ad terram tenebrosam, et opertam mortis caligine:
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 terram miseriæ et tenebrarum, ubi umbra mortis et nullus ordo, sed sempiternus horror inhabitat.]
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >