< Mateu 13 >

1 Helyo izuva Jesu avayendi hanze yenzuoo ni kukala kwimbali ye wate.
Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
2 Inyangela inkando iva kopene kumuzimbuluka, chechila mu chisepe ni kwikala mwateni. Inyangela yonse iva zimene helizo.
Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
3 Linu Jesu chawamba zintu zingi kuvali mwi nguli. Chati, “Muvone, mubyali avayendi kukubyila.
Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
4 Haba kukavubyala vulyo, imwi umbuto chiyawila kwimbali yenzila, mi zizuni chizakeza chizeza kuilya.
Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
5 Imwi imbuto iba wili mwivu lya mabwe, uko kuisena iva wani ivu ilingi. Haho fele chiya mena, kakuti ivu kena livatungite.
Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
6 Kono izuva hali tanta, zivamenete chiza letuka kakuli kena zivena mihisi, mi chizazuma.
Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
7 Imwi imbuko iva wili mu kati kezi samu. Masamu amwiya chia kula ni kuzi puputiza,
Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
8 Imwi imbuto iba wili mwivu lina hande mi ziva biki vuheke, amwi makumi e kumi nikuhitilila, amwi makumi amana iyanza ni limwina, amwi makumi otatwe.
Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
9 Eye yo zuwa, mumusiye atekeleze.
Aliye na masikio na asikie.
10 Valutwana chivakeza ni chivati kwa Jesu, “Chinzi howamba kwi nyangela mwinguli?”
Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
11 Jesu chetava ni chati kuvali, “Muvahewa inswenelo yaku zuwisisa inkunutu zamuvuso wa kwiulu, kono kuvali kena kevava hewa.
Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
12 Kakuti yense yo wina, kwali kahewe zingi, mi kakwi zule kwali. Kono yense ya sena, kwali kanyangwe ni chakwete.
Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
13 Cwale niwamba kubali che nguli, kakuti ni haike vavona, kava vonisisi. Mi nihava zuwa vulyo, kavazuwi, mikava zuwisisi.
Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
14 Kuvali chipolofita cha Isaya chivezuzilizwa, chita kuti, 'Chotekeleze uzuwa kono kete uzuwisise, chololete uvona, kono kete uvonisise.
Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
15 kakuti vantu inkulo zavo chiza nuna, mi vakukutu kuzuwa, mi vave yali menso avo, ili kiti senzi vavoni ni menso avo, kapa kuzuwa chamatwi avo, kapa kuzuwisisa che nkulo zavo, ili kuti vasandumuke hape, mi nini vavahozi.'
Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
16 Kono chi tonofezwe menso enu, kuti avone; ni matwi enu, kuti azuwe.
Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
17 Cheniti ni miwambila kuti vungu bwa vapolofita ni vantu valukite vatavela kuvona zintu zimuvona, mi kana vavaziboni. Vatabela kuzuwa zintu zimuzuwa, mi kana vavazizuwi.
Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
18 Muteke kwi nguli ya mubyali.
. Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
19 Linu yense muntu hazuwa linzwi lya muvuso kono kali zuwisisi, haho vantu vavi vakeza kwiza kuhinda cha byalite mwi nkulo yakwe. Iyi nji mbuto iva byaliwe kwimbali ye nzila.
Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
20 Iye yava byalwa hevu lya mabwe njo zuwa linzwi ni kulitambula cho kusanga haho.
Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
21 Mi kena mihisi iye mwine kono ukwata vulyo inako zana. Linu manyando kapa kwihaiwa chikwava kwateni chevaka lye nzi, ka sitatale njiho haho.
Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
22 Yavabyila mukati ke zisamu zamiya, uzu njiyena yozuwa linzi, kono kuvilelela ifasi nikusaka ahulu chifuma zi sina linzwi ni kusaha miselo. (aiōn g165)
Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
23 Yavabyilwa he ivu ilotu, uzu njo zuwa linzwi nikuli zuwisisa. Uzu njo vikava miselo, ni yoilima; imwi makumi a kumi nikuhitilila, imwi mashumi akwanisa iyanza ni lyonke, imwi makumi otatwe.
Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
24 Jesu chavaha imwi inguli. Chati. “Muso wa kwiwuulu ukola sina ili muntu yabyali intanga zilotu mwiwa lyakwe.
Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
25 Kono vantu nivalele, zila zakwe nazo chizakeza kubya mumukula mukati ka vuloto ni kuyenda.
Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
26 Linu vuloto havukula mena ni kuvika miselo mukula nawo chiwavoneka.
Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
27 Valeki vamwine waluwa chivakeza chivati kwali, 'Unkoshangu, kena uvabyali intanga zina hande muluwa lwako? Chinzi hachikuwanika mukula?'
Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
28 Chati kuvali, 'Yonitoyete nja vapangi vulyo,' Vatanga vakwe chivati kwali, 'Cwale usaka kuti tuka zinyukule mwateni?'
Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
29 Mwina luwa chati, 'Nee, kakuti chi mwakanyukula mwateni mukula, pona chimuka nyukulilila ni vuloto.
Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
30 Muzisiye zikulille hamwina kulindila inkutulo. He nako ye nkutulo kaniwambe kuva kutuli, “Chentanzi munyukolo mukula ni kuisumina mañata kuti uhisiwe, kono mukunganye vuloto muzishete zangu.'””
Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
31 Jesu chawamba imwi inguli kuvali, chati, “Muvuso wa kwiul ukola sina intanga ya masitete iyo muntu yavahindi ni kubyala muluwa lwakwe.
Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
32 Iyi imbuto inini kwimbuto zonse. Kono haiva ya byalwa hande, inkando kuzi chalano za muluwa. Ikula iva isamu, mi zizuni ze wulu zikeza kuzaka zizumbo kumitayi yalyo.
Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
33 Jesu linu chavawambila imwi inguli. “Muvuso wakwiulu ukola ili chivilisa icho mwanakazi avahindi ni kukopanya ni ntikanyo zo tatwe za busu konji hakufunduluka.”
Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
34 Zonse inzi zintu Jesu avaziwambi kwinyangela mwinguli. Mi kwanda yenguli kakwina chavawambi kuvali.
Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
35 Iyi ivavi intaelo kuti chonse chiva vawambwa chamupolofita chiwola kuba init. Haho chati, “kaniyalule kaholo kangu mwinguli. Kani wambe zintu zibapatitwe kuzwa kumatangizo inkanda.
Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
36 Linu Jesu chasiya chichava nikuya mwinzuvo. Valutwana bakwe chivakeza kwali mi chivati, “Tutolokele inguli ya mufuka mwiwa.”
Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
37 Jesu chetaba chati, “Yababyali intanga zina hande Mwana wa Mulimu.
Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
38 Luwa inkanda; Mi intanga zina hande, izi vana va mubuso, mufuka vana va satani.
Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
39 Mi chila chivazibyali nji diavulusi. Inkutulo njimamanimani e nkanda, bakutuli mañiloyi. (aiōn g165)
Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 Hakuva vulyo, mukula kaukunganye nikuhiswa chamulilo, njete kuve njimamanimani e nkanda. (aiōn g165)
Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
41 Mwana muntu ka tumine mañiloi akwe, mikava kunganyeze hanze ya muvuso zintu zonse zileta chivi, niva vapanga vulilala.
Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
42 Kavava sohele mwilyanga lilo, uko kavakalile nikukwecha meeno.
Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43 Linu bantu balukite kavavenye sina izuva mumubuso weshevo. Iye yowina matwi, musiye atekeleze.
Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
44 Muvuso wa kwiulu ukola ili ibwe lya butokwa lipatitwe muluwa. Muntu abaliwan mi chalipata. Mwintavo ya kwe chayenda, ku uza zintu zonse zavakwete, nikuula ulo luwa.
Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
45 Hape muvuso wa Mulimu ukola ili muntu yo patehete kukavulola mabwe abutokwa.
Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
46 Hawana ibwe lina maemo ena hande, avayendi nikukauza zintu zakwe zonse zava kwete nikuliula.
Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
47 Hape, muvuso wa kwiulu ukola ili kanyandi kavasohelwa mwi wate, kavachesi mufutafuta ye zintu.
Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
48 Linu hakezula, muyambi chaka kwitila hamutunda. Linu chivekala hansi ni ku kunganya zintu zilotu muchiseye, mi zintu zivi zivasohelwa kwimbali.
Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
49 Mukuve mweyi inzila kumamanimani inkanda. Mañiloi muakeze kukauhanya vavi mukati ka vantu valukite. (aiōn g165)
Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
50 Kavava sohele mwi bimbililo lya mulilo, kwete vakahye niku kwecha meeno.
Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
51 Mwazizuwisisa nzose izi zintu?” Valutwana chivati kwali, “Eni, “
Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
52 Linu Jesu chati kuvali, “Hakuva vulyo vañoli vonse vavavi valutwana ku muvuso weulu vaswa ili nji muntu yeli mwine we nzuvo. Yozwisa zakale ni zintu zihya muchifumu chakwe.”
Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
53 Linu nichiya keza kuva vulyo Jesu hamana izi inguli, cha katuka kuzwa mwe chochivaka.
IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
54 Linu Jesu che njila muchi kiliti chakwe ni kuluta vantu mumasinagoge avo. Inkalavo ivali kukomokwa ni kuti, “Kanti uzu mutu uwana kuhi vutali ne zi imakazo kuhi?
Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
55 Uzu muntu kena mwana wa muvezi? Kena vanyina nji Maria? Ni vanche kena nji Jamusi, Josefa, Simone ni Judasi?
Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
56 Ni vanchizya kwe kavakwina mukati ketu? Cwale uzu muntu uwana kuhi zonse izi zintu?”
Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
57 Vava vengwiswa kwali. Kono Jesu chati kuvali, “Mupolofita uswanela kukutekiwa kuunde mwinkanda yakwe ni kuvaluhasi lwakwe.
Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
58 Mi kena ava pangi imakazo zingi kwateni chevaka lyakuvula intumelo.
Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.

< Mateu 13 >