< Oekyuk 33 >

1 Ma simla inge fahkak inen acn ma mwet Israel aktuktuk we tukun elos fahsr liki acn Egypt ke sruf lalos ye kolyuk lal Moses ac Aaron.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Moses el simusla inen kais sie acn ma elos tulokunak lohm nuknuk selos we, oana ma LEUM GOD El sapkin.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Mwet Israel elos som liki Egypt ke len aksingoul limekosr in malem se meet in yac, len se tukun Kufwen Alukela se oemeet. Ye karinginyuk lun LEUM GOD elos illa liki siti Rameses ye mutun mwet Egypt,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 su pikin wounse mukul natulos ma LEUM GOD El uniya. LEUM GOD El oru ouinge in akkalemye lah El arulana ku liki god lun acn Egypt.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Mwet Israel som liki acn Rameses ac tulokunak nien aktuktuk lalos Sukkoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Nien aktuktuk lalos akluo pa in acn Etham sisken yen mwesis.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Liki acn sac elos folokla nu Pi Hahiroth, kutulap in Baal Zephon, ac aktuktuk apkuran nu Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Elos mukuila liki Pi Hahiroth ac fahsr sasla in Meoa Srusra nu in acn mwesis lun Shur. Tukun fahsr ke len tolu elos aktuktuk in acn Marah.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Liki acn we elos som nu Elim ac aktuktuk we, mweyen oasr unon in kof singoul luo ac sak palm itngoul we.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Elos fahsr liki Elim ac aktuktuk apkuran nu ke Meoa Srusra.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Acn in aktuktuk se lalos toko pa yen mwesis lun Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Na toko elos aktuktuk Dophkah,
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 ac toko in acn Alush,
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 ac toko in acn Rephidim, acn se ma wangin kof elos in nim we.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Elos mukuiyak liki acn Rephidim ac som aktuktuk in acn mwesis lun Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Elos som liki acn we nu in acn Kibroth Hattaavah.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Tok elos som ac aktuktuk in kais sie acn inge: Hazeroth,
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Rithmah,
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Rimmon Perez,
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Libnah,
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Rissah,
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Kehelathah,
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Eol Shepher,
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Haradah,
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Makheloth,
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Tahath,
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Terah,
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Mithkah,
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Hashmonah,
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Moseroth,
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Bene Jaakan,
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Hor Haggidgad,
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Jotbathah,
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Abronah,
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Ezion Geber,
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 acn mwesis lun Zin (pa ingan acn Kadesh),
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 ac Eol Hor, sisken na facl Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Aaron mwet tol el fanyak nu fin mangon Eol Hor, oana ke LEUM GOD El sapkin nu sel, ac el misa we ke len se oemeet in malem se aklimekosr ke yac akangngaul tukun mwet Israel elos illa liki acn Egypt.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron el yac siofok longoul tolu ke el misa Fineol Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 Tokosra lun Arad, su oan layen eir in acn Canaan, el lohngak lah mwet Israel apkuranme.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Mwet Israel elos mukuiyak liki Eol Hor ac aktuktuk Zalmonah.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Na toko elos aktuktuk ke kais sie acn inge: Punon,
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Oboth,
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 mahnum Abarim in acn Moab,
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Dibon Gad,
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Almon Diblathaim,
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Fineol Abarim, apkuran nu Fineol Nebo,
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 ac in acn tupasrpasr Moab su oan layen kutulap in Infacl Jordan tulanang Jericho,
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 inmasrlon Beth Jeshimoth na nwe infahlfal Acacia in acn mwesis lun Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 In acn mwesis lun Moab sisken Infacl Jordan tulanang acn Jericho, LEUM GOD El kaskas nu sel Moses ac fahk,
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 “Kaskas nu sin mwet Israel, ac fahk nu selos: Pacl se kowos fahsr alukela Infacl Jordan ac utyak nu in facl Canaan,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 kowos in lusak mwet nukewa we. Kunausla ma sruloala lalos nukewa — ma orekla ke eot ac ma orekla ke osra — wi acn in alu lalos nukewa.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Sruokya facl sac ac oakwuki we, mweyen nga sot acn we tuh in ma suwos.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Kitalik acn we ke fa, nu sin sruf ac sou lowos nukewa. Sang ipin acn ma yohk nu sin sruf ma yohk, ac ipin acn ma srik nu sin sruf ma srik.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Kowos fin tia lusla mwet nukewa su muta we, na mwet lula uh ac fah arulana aklokoalokye kowos, oana kutkut in atronmotowos, ku oana sak ma oasr otoh kac inpupowos, na tok elos ac foroht lain kowos.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Kowos fin tia luselosla, na nga ac kunauskowosla oana ke nga akoo in kunauselosla.”
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Oekyuk 33 >