< Oekyuk 33 >

1 Ma simla inge fahkak inen acn ma mwet Israel aktuktuk we tukun elos fahsr liki acn Egypt ke sruf lalos ye kolyuk lal Moses ac Aaron.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Moses el simusla inen kais sie acn ma elos tulokunak lohm nuknuk selos we, oana ma LEUM GOD El sapkin.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Mwet Israel elos som liki Egypt ke len aksingoul limekosr in malem se meet in yac, len se tukun Kufwen Alukela se oemeet. Ye karinginyuk lun LEUM GOD elos illa liki siti Rameses ye mutun mwet Egypt,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 su pikin wounse mukul natulos ma LEUM GOD El uniya. LEUM GOD El oru ouinge in akkalemye lah El arulana ku liki god lun acn Egypt.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Mwet Israel som liki acn Rameses ac tulokunak nien aktuktuk lalos Sukkoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Nien aktuktuk lalos akluo pa in acn Etham sisken yen mwesis.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Liki acn sac elos folokla nu Pi Hahiroth, kutulap in Baal Zephon, ac aktuktuk apkuran nu Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Elos mukuila liki Pi Hahiroth ac fahsr sasla in Meoa Srusra nu in acn mwesis lun Shur. Tukun fahsr ke len tolu elos aktuktuk in acn Marah.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Liki acn we elos som nu Elim ac aktuktuk we, mweyen oasr unon in kof singoul luo ac sak palm itngoul we.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Elos fahsr liki Elim ac aktuktuk apkuran nu ke Meoa Srusra.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Acn in aktuktuk se lalos toko pa yen mwesis lun Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Na toko elos aktuktuk Dophkah,
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 ac toko in acn Alush,
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 ac toko in acn Rephidim, acn se ma wangin kof elos in nim we.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Elos mukuiyak liki acn Rephidim ac som aktuktuk in acn mwesis lun Sinai.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Elos som liki acn we nu in acn Kibroth Hattaavah.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Tok elos som ac aktuktuk in kais sie acn inge: Hazeroth,
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Rithmah,
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Rimmon Perez,
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Libnah,
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Rissah,
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Kehelathah,
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Eol Shepher,
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Haradah,
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Makheloth,
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Tahath,
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Terah,
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Mithkah,
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Hashmonah,
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Moseroth,
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Bene Jaakan,
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Hor Haggidgad,
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Jotbathah,
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Abronah,
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Ezion Geber,
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 acn mwesis lun Zin (pa ingan acn Kadesh),
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 ac Eol Hor, sisken na facl Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Aaron mwet tol el fanyak nu fin mangon Eol Hor, oana ke LEUM GOD El sapkin nu sel, ac el misa we ke len se oemeet in malem se aklimekosr ke yac akangngaul tukun mwet Israel elos illa liki acn Egypt.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aaron el yac siofok longoul tolu ke el misa Fineol Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Tokosra lun Arad, su oan layen eir in acn Canaan, el lohngak lah mwet Israel apkuranme.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Mwet Israel elos mukuiyak liki Eol Hor ac aktuktuk Zalmonah.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Na toko elos aktuktuk ke kais sie acn inge: Punon,
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Oboth,
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 mahnum Abarim in acn Moab,
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Dibon Gad,
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Almon Diblathaim,
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Fineol Abarim, apkuran nu Fineol Nebo,
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 ac in acn tupasrpasr Moab su oan layen kutulap in Infacl Jordan tulanang Jericho,
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 inmasrlon Beth Jeshimoth na nwe infahlfal Acacia in acn mwesis lun Moab.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 In acn mwesis lun Moab sisken Infacl Jordan tulanang acn Jericho, LEUM GOD El kaskas nu sel Moses ac fahk,
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 “Kaskas nu sin mwet Israel, ac fahk nu selos: Pacl se kowos fahsr alukela Infacl Jordan ac utyak nu in facl Canaan,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 kowos in lusak mwet nukewa we. Kunausla ma sruloala lalos nukewa — ma orekla ke eot ac ma orekla ke osra — wi acn in alu lalos nukewa.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Sruokya facl sac ac oakwuki we, mweyen nga sot acn we tuh in ma suwos.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Kitalik acn we ke fa, nu sin sruf ac sou lowos nukewa. Sang ipin acn ma yohk nu sin sruf ma yohk, ac ipin acn ma srik nu sin sruf ma srik.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Kowos fin tia lusla mwet nukewa su muta we, na mwet lula uh ac fah arulana aklokoalokye kowos, oana kutkut in atronmotowos, ku oana sak ma oasr otoh kac inpupowos, na tok elos ac foroht lain kowos.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Kowos fin tia luselosla, na nga ac kunauskowosla oana ke nga akoo in kunauselosla.”
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Oekyuk 33 >