< Ezra 8 >

1 Pa inge inen sifen sou su muta in sruoh in Babylonia ac welul Ezra folokla nu Jerusalem ke pacl Artaxerxes el tokosra fulat:
Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
2 Gershom ke fwil natul Phinehas Daniel ke fwil natul Ithamar Hattush, wen natul Shecaniah, ke fwil natul David
wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
3 Zechariah ke fwil natul Parosh wi mwet 150 ke sou lulap lal (simisyukla inen mwet in sou lalos ke sramsram matu)
wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
4 Eliehoenai, wen natul Zerahiah, ke fwil natul Pahath Moab, wi mukul 200
wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
5 Shecaniah, wen natul Jahaziel, ke fwil natul Zattu, wi mukul 300
wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
6 Ebed, wen natul Jonathan, ke fwil natul Adin, wi mukul 50
wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
7 Jeshaiah, wen natul Athaliah, ke fwil natul Elam, wi mukul 70
wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
8 Zebadiah, wen natul Michael, ke fwil natul Shephatiah, wi mukul 80
wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
9 Obadiah, wen natul Jehiel, ke fwil natul Joab, wi mukul 218
wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
10 Shelomith, wen natul Josiphiah, ke fwil natul Bani, wi mukul 160
wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
11 Zechariah, wen natul Bebai, ke fwil natul Bebai, wi mukul 28
wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
12 Johanan, wen natul Hakkatan, ke fwil natul Azgad, wi mukul 110
wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
13 Eliphelet, Jeuel, ac Shemaiah ke fwil natul Adonikam, wi mukul 60, (elos folokla ke sie pacl tok)
wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
14 Uthai ac Zaccur ke fwil natul Bigvai, wi mukul 70
wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
15 Nga orani u nufon sac nu pe inyoa soko ma sasla nu Ahava, ac kut aktuktuk we len tolu. Nga konauk lah oasr mwet tol in u sac, a wangin mwet Levi.
Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
16 Nga sapla suli eu sin mwet kol lalos: Eliezer, Ariel, Shemaiah, Elnathan, Jarib, Elnathan, Nathan, Zechariah, ac Meshullam, oayapa luo mwet luti: Joiarib ac Elnathan.
Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
17 Nga supwalosla nu yorol Iddo, su leumi acn Casiphia, in siyuk sel ac mwet kasru lal su orekma ke Tempul, tuh elos in supwama mwet in kulansap nu sin God in Tempul.
nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
18 Ke lungkulang lun God, elos supwalma Sherebiah, sie mwet fas, su mwet Levi se in fwil natul Mahli; ac mukul singoul oalkosr sin wen natul ac tamulel lal welul tuku.
Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
19 Elos oayapa supwalma Hashabiah ac Jeshaiah ke fwil natul Merari, wi mwet longoul sin mwet laltal.
Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
20 Sayen mwet inge, oasr luofoko longoul mwet orekma ke Tempul su mwet matu lalos tuh srisrngiyuki sel Tokosra David ac mwet pwapa lal tuh elos in kasru mwet Levi. Simisyukla inelos kais sie.
Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
21 Ingo sisken Inyoa Ahava, nga sapkin tuh kut nukewa in lalo ac akpusiselye kut ye mutun God lasr, ac siyuk sel tuh Elan kol kut ke fahsr lasr ac lisringkuti ac tulik natusr ac ma lasr nukewa.
Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
22 Nga lukun mwekin in siyuk sin tokosra fulat ke sie u in mwet mweun ma kasrusr fin horse in karingin kut ke fufahsryesr lasr liki kutena mwet lokoalok, mweyen nga fahk nu sel tari lah God lasr El akinsewowoyalos nukewa su lulalfongi El, a El lain ac kalyei kutena su forla lukel.
Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
23 Ouinge kut lalo ac pre tuh God Elan karingin kut, ac El topuk pre lasr.
Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
24 Inmasrlon mwet tol su fulat, nga tuh sulella Sherebiah, Hashabiah, ac mwet singoul saya.
Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
25 Na nga pauniya silver, gold ac ahlu in kulansap ma tokosra fulat, mwet pwapa ac mwet fulat lal oayapa mwet Israel nukewa elos tuh sang in orekmakinyuk in Tempul, ac nga sang nu sin mwet tol.
nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
26 Pa inge ma nga sang nu selos: silver — ton 25 100 ahlu silver, kufwen mwe orekma — paun 150 gold — paun 7,500
Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
27 20 ahlu gold — paun 16 tafu 2 ahlu bronze wowo — lupan molo uh oana molin ahlu gold.
mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
28 Nga fahk nu selos, “Kowos mutal ye mutun LEUM GOD lun mwet matu lowos, ac oayapa ahlu silver ac gold su itukyang nu sel ke insewowo, ma inge mutal pac.
Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
29 Kowos karinganang akwoya nwe ke kowos sun Tempul. Kowos pauniya ma inge infukil lun mwet tol, ac sang nu sin mwet kol lun mwet tol ac mwet Levi, ac nu sin mwet kol lun Israel in Jerusalem.”
Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
30 Ke ma inge mwet tol ac mwet Levi elos eis ac fosrngakin silver, gold, ac kufwen mwe orekma, ac elos usla nu in Tempul Jerusalem.
Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
31 Len se aksingoul luo ke malem se meet pa kut mukuiyak liki Inyoa Ahava in som nu Jerusalem. God lasr El wi kut ac karingin kut liki mwet lokoalok ac liki mwet su akola in kasriki kut inkanek ah.
Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
32 Ke kut sun acn Jerusalem, kut muta mongla len tolu.
Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
33 Na len se akakosr kut som nu ke Tempul, pauniya silver, gold, ac kufwen mwe orekma, na kut sang nu sel Meremoth mwet tol, wen natul Uriah. Mwet tolu welul pa: Eleazar wen natul Phinehas, ac mwet Levi luo, Jozabad wen natul Jeshua, ac Noadiah wen natul Binnui.
Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
34 Ma nukewa oaoala ac paunyuki, ac simla in pacl sac pacna.
Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
35 Na mwet nukewa su foloko liki sruoh elos use mwe sang lalos tuh in mwe kisa firir nu sin God lun Israel. Elos sang cow mukul 12 ke Israel nufon, wi sheep mukul 96, ac sheep fusr 77. Elos oayapa sang nani 12 mwe aknasnasyalos liki ma koluk. Ma inge nukewa mwe kisa firir nu sin LEUM GOD.
Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
36 Elos oayapa usla leta se ma tokosra fulat el tuh sang nu selos ac sang nu sel governor ac mwet pwapa lun acn Roto-in-Euphrates, na mwet inge elos oru pac kasru lalos nu sin mwet uh ac nu ke alu in Tempul.
Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.

< Ezra 8 >