< 욥기 27 >

1 욥이 또 비사를 들어 가로되
Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 나의 의를 빼앗으신 하나님 나의 영혼을 괴롭게 하신 전능자의 사심을 가리켜 맹세하노니
“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, Mwenyezi ambaye amenifanya nionje uchungu wa nafsi,
3 (나의 생명이 아직 내 속에 완전히 있고 하나님의 기운이 오히려 내 코에 있느니라)
kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
4 결코 내 입술이 불의를 말하지 아니하며 내 혀가 궤휼을 발하지 아니하리라
midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5 나는 단정코 너희를 옳다 하지 아니하겠고 죽기 전에는 나의 순전함을 버리지 않을 것이라
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6 내가 내 의를 굳게 잡고 놓지 아니하리니 일평생 내 마음이 나를 책망치 아니하리라
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7 나의 대적은 악인 같이 되고 일어나 나를 치는 자는 불의한 자 같이 되기를 원하노라
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
8 사곡한 자가 이익을 얻었으나 하나님이 그 영혼을 취하실 때에는 무슨 소망이 있으랴
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
9 환난이 그에게 임할 때에 하나님이 어찌 그 부르짖음을 들으시랴
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
10 그가 어찌 전능자를 기뻐하겠느냐 항상 하나님께 불러 아뢰겠느냐
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
11 하나님의 하시는 일을 내가 너희에게 가르칠 것이요 전능자의 뜻을 내가 숨기지 아니하리라
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
12 너희가 다 이것을 보았거늘 어찌하여 아주 허탄한 사람이 되었는고
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
13 악인이 하나님께 얻을 분깃, 강포자가 전능자에게 받을 산업은 이것이라
“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
14 그 자손이 번성하여도 칼을 위함이요 그 후예는 식물에 배부르지 못할 것이며
Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani, fungu lao ni kuuawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa kamwe na chakula cha kuwatosha.
15 그 남은 자는 염병으로 묻히리니 그의 과부들이 울지 못할 것이며
Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, nao wajane wao hawatawaombolezea.
16 그가 비록 은을 티끌 같이 쌓고 의복을 진흙 같이 예비할지라도
Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
17 그 예비한 것을 의인이 입을 것이요 그 은은 무죄자가 나눌 것이며
yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
18 그 지은 집은 좀의 집 같고 상직군의 초막 같을 것이며
Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
19 부자로 누우나 그 조상에게로 돌아가지 못할 것이요 눈을 뜬즉 없어졌으리라
Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.
20 두려움이 물 같이 그를 따라 미칠 것이요 폭풍이 밤에 그를 빼앗아갈 것이며
Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.
21 동풍이 그를 날려 보내며 그 처소에서 몰아 내리라
Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.
22 하나님이 그를 아끼지 아니하시고 쏘시나니 그가 그 손에서 피하려 하여도 못할 것이라
Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
23 사람들이 박장하며 비소하고 그 처소에서 몰아내리라
Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.

< 욥기 27 >