< 욥기 20 >
Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2 그러므로 내 생각이 내게 대답하나니 이는 내 중심이 초급함이니라
“Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu, kwa sababu nimehangaika sana.
3 내가 나를 부끄럽게 하는 책망을 들었으므로 나의 슬기로운 마음이 내게 대답하는구나
Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima, nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.
4 네가 알지 못하느냐 예로부터 사람이 이 세상에 있어 옴으로
“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
5 악인의 이기는 자랑도 잠시요 사곡한 자의 즐거움도 잠간이니라
macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
6 그 높기가 하늘에 닿고 그 머리가 구름에 미칠지라도
Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
7 자기의 똥처럼 영원히 망할 것이라 그를 본 자가 이르기를 그가 어디 있느냐 하리라
ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
8 그는 꿈 같이 지나가니 다시 찾을 수 없을 것이요 밤에 보이던 환상처럼 쫓겨가리니
Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
9 그를 본 눈이 다시 그를 보지 못할 것이요 그의 처소도 다시 그를 보지 못할 것이며
Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
10 그의 자녀들이 가난한 자에게 은혜를 구하겠고 그도 얻은 재물을 자기 손으로 도로 줄 것이며
Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.
11 그 기골이 청년 같이 강장하나 그 기세가 그와 함께 흙에 누우리라
Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
12 그는 비록 악을 달게 여겨 혀 밑에 감추며
“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
13 아껴서 버리지 아니하고 입에 물고 있을지라도
ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
14 그 식물이 창자 속에서 변하며 뱃속에서 독사의 쓸개가 되느니라
Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.
15 그가 재물을 삼켰을지라도 다시 토할 것은 하나님이 그 배에서 도로 나오게 하심이니
Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.
16 그가 독사의 독을 빨며 뱀의 혀에 죽을 것이라
Atanyonya sumu za majoka; meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.
17 그는 강 곧 꿀과 엉긴 젖이 흐르는 강을 보지 못할 것이요
Hatafurahia vijito, mito inayotiririsha asali na siagi.
18 수고하여 얻은 것을 도로 주고 삼키지 못할 것이며 매매하여 얻은 재물로 즐거워하지 못하리니
Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila; hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.
19 이는 그가 가난한 자를 학대하고 버림이요 자기가 세우지 않은 집을 빼앗음이니라
Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu; amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.
20 그는 마음에 족한 줄을 알지 못하니 그 기뻐하는 것을 하나도 보존치 못하겠고
“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana; hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.
21 남긴 것이 없이 몰수히 먹으니 그런즉 그 형통함이 오래지 못할 것이라
Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale; kufanikiwa kwake hakutadumu.
22 풍족할 때에도 곤액이 이르리니 모든 고통하는 자의 손이 그에게 닿으리라
Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.
23 그가 배를 불리려 할 때에 하나님이 맹렬한 진노를 내리시리니 밥 먹을 때에 그의 위에 비 같이 쏟으시리라
Atakapokuwa amelijaza tumbo lake, Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake, na kumnyeshea mapigo juu yake.
24 그가 철병기를 피할 때에는 놋활이 쏘아 꿸 것이요
Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma, mshale wa shaba utamchoma.
25 몸에서 그 살을 빼어 낸즉 번쩍번쩍하는 촉이 그 쓸개에서 나오고 큰 두려움이 그에게 임하느니라
Atauchomoa katika mgongo wake, ncha ingʼaayo kutoka ini lake. Vitisho vitakuja juu yake;
26 모든 캄캄한 것이 그의 보물을 위하여 쌓이고 사람이 피우지 않은 불이 그를 멸하며 그 장막에 남은 것을 사르리라
giza nene linavizia hazina zake. Moto usiopepewa na mtu utamteketeza, na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.
27 하늘이 그의 죄악을 드러낼 것이요 땅이 일어나 그를 칠 것인즉
Mbingu zitaweka wazi hatia yake, nayo nchi itainuka kinyume chake.
28 그 가산이 패하여 하나님의 진노하시는 날에 흘러가리니
Mafuriko yataichukua nyumba yake, maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
29 이는 악인이 하나님께 받을 분깃이요 하나님이 그에게 정하신 산업이니라
Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu, urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”