< 창세기 10 >
1 노아의 아들 셈과 함과 야벳의 후예는 이러하니라 홍수 후에 그들이 아들들을 낳았으니
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 야벳의 아들은 고멜과 마곡과 마대와 야완과 두발과 메섹과 디라스요
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 고멜의 아들은 아스그나스와 리밧과 도갈마요
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 야완의 아들은 엘리사와 달시스와 깃딤과 도다님이라
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 이들로부터 여러 나라 백성으로 나뉘어서 각기 방언과 종족과 나라대로 바닷가의 땅에 머물렀더라
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 함의 아들은 구스와 미스라임과 붓과 가나안이요
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 구스의 아들은 스바와 하윌라와 삽다와 라아마와 삽드가요 라아마의 아들은 스바와 드단이며
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 구스가 또 니므롯을 낳았으니 그는 세상에 처음 영걸이라
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 그가 여호와 앞에서 특이한 사냥꾼이 되었으므로 속담에 이르기를 아무는 여호와 앞에 니므롯 같은 특이한 사냥꾼이로다 하더라
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 그의 나라는 시날 땅의 바벨과 에렉과 악갓과 갈레에서 시작되었으며
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 그가 그 땅에서 앗수르로 나아가 니느웨와 르호보딜과 갈라와
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 및 니느웨와 갈라 사이의 레센(이는 큰 성이라)을 건축하였으며
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 미스라임은 루딤과 아나밈과 르하빔과 납두힘과
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 바드루심과 가슬루힘과 갑도림을 낳았더라 (블레셋이 가슬루힘에게서 나왔더라)
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 또 여부스 족속과 아모리 족속과 기르가스 족속과
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
18 아르왓 족속과 스말 족속과 하맛 족속의 조상을 낳았더니 이 후로 가나안 자손의 족속이 흩어져 처하였더라
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 가나안의 지경은 시돈에서부터 그랄을 지나 가사까지와 소돔과 고모라와 아드마와 스보임을 지나 라사까지였더라
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 이들은 함의 자손이라 각기 족속과 방언과 지방과 나라대로이었더라
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 셈은 에벨 온 자손의 조상이요 야벳의 형이라 그에게도 자녀가 출생하였으니
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 셈의 아들은 엘람과 앗수르와 아르박삿과 룻과 아람이요
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 아람의 아들은 우스와 훌과 게델과 마스며
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 아르박삿은 셀라를 낳고 셀라는 에벨을 낳았으며
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 에벨은 두 아들을 낳고 하나의 이름을 벨렉이라 하였으니 그 때에 세상이 나뉘었음이요 벨렉의 아우의 이름은 욕단이며
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 욕단은 알모닷과 셀렙과 하살마웹과 예라와
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
29 오빌과 하윌라와 요밥을 낳았으니 이들은 다 욕단의 아들이며
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 그들의 거하는 곳은 메사에서부터 스발로 가는 길의 동편 산이었더라
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 이들은 셈의 자손이라 그 족속과 방언과 지방과 나라대로였더라
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 이들은 노아 자손의 족속들이요 그 세계와 나라대로라 홍수 후에 이들에게서 땅의 열국백성이 나뉘었더라
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.