< 시편 8 >

1 (다윗의 시. 영장으로 깃딧에 맞춘 노래) 여호와 우리 주여, 주의 이름이 온 땅에 어찌 그리 아름다운지요 주의 영광을 하늘 위에 두셨나이다
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Umeuweka utukufu wako juu ya mbingu.
2 주의 대적을 인하여 어린 아이와 젖먹이의 입으로 말미암아 권능을 세우심이여 이는 원수와 보수자로 잠잠케 하려 하심이니이다
Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa, kwa sababu ya watesi wako, kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.
3 주의 손가락으로 만드신 주의 하늘과 주의 베풀어 두신 달과 별들을 내가 보오니
Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota, ulizoziratibisha,
4 사람이 무엇이관대 주께서 저를 권고하시나이까
mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
5 저를 천사보다 조금 못하게 하시고 영화와 존귀로 관을 씌우셨나이다
Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni, ukamvika taji ya utukufu na heshima.
6 주의 손으로 만드신 것을 다스리게 하시고 만물을 그 발 아래 두셨으니
Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako; umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.
7 곧 모든 우양과 들짐승이며
Mifugo na makundi yote pia, naam, na wanyama wa kondeni,
8 여호와 우리 주여, 주의 이름이 온 땅에 어찌 그리 아름다운지요
ndege wa angani na samaki wa baharini, naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.
9
Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

< 시편 8 >