< 시편 78 >

1 (아삽의 마스길) 내 백성이여, 내 교훈을 들으며 내 입의 말에 귀를 기울일지어다
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 내가 입을 열고 비유를 베풀어서 옛 비밀한 말을 발표하리니
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 이는 우리가 들은 바요 아는 바요 우리 열조가 우리에게 전한 바라
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 우리가 이를 그 자손에게 숨기지 아니하고 여호와의 영예와 그 능력과 기이한 사적을 후대에 전하리로다
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 여호와께서 증거를 야곱에게 세우시며 법도를 이스라엘에게 정하시고 우리 열조에게 명하사 저희 자손에게 알게 하라 하셨으니
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 이는 저희로 후대 곧 후생 자손에게 이를 알게 하고 그들은 일어나 그 자손에게 일러서
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 저희로 그 소망을 하나님께 두며 하나님의 행사를 잊지 아니하고 오직 그 계명을 지켜서
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 그 열조 곧 완고하고 패역하여 그 마음이 정직하지 못하며 그 심령은 하나님께 충성치 아니한 세대와 같지 않게 하려 하심이로다
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 에브라임 자손은 병기를 갖추며 활을 가졌으나 전쟁의 날에 물러갔도다
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 저희가 하나님의 언약을 지키지 아니하고 그 율법 준행하기를 거절하며
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 여호와의 행하신 것과 저희에게 보이신 기사를 잊었도다
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 옛적에 하나님이 애굽 땅 소안 들에서 기이한 일을 저희 열조의 목전에서 행하셨으되
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 저가 바다를 갈라 물을 무더기 같이 서게 하시고 저희로 지나게 하셨으며
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 낮에는 구름으로 온 밤에는 화광으로 인도하셨으며
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 광야에서 반석을 쪼개시고 깊은 수원에서 나는 것 같이 저희에게 물을 흡족히 마시우셨으며
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 또 반석에서 시내를 내사 물이 강 같이 흐르게 하셨으나
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 저희는 계속하여 하나님께 범죄하여 황야에서 지존자를 배반하였도다
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 저희가 저희 탐욕대로 식물을 구하여 그 심중에 하나님을 시험하였으며
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 그 뿐 아니라 하나님을 대적하여 말하기를 하나님이 광야에서 능히 식탁을 준비하시랴
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 저가 반석을 쳐서 물을 내시매 시내가 넘쳤거니와 또 능히 떡을 주시며 그 백성을 위하여 고기를 예비하시랴 하였도다
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 그러므로 여호와께서 듣고 노하심이여 야곱을 향하여 노가 맹렬하며 이스라엘을 향하여 노가 올랐으니
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 이는 하나님을 믿지 아니하며 그 구원을 의지하지 아니한 연고로다
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 그러나 저가 오히려 위의 궁창을 명하시며 하늘 문을 여시고
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 저희에게 만나를 비같이 내려 먹이시며 하늘 양식으로 주셨나니
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 사람이 권세 있는 자의 떡을 먹음이여 하나님이 식물을 충족히 주셨도다
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 저가 동풍으로 하늘에서 일게 하시며 그 권능으로 남풍을 인도하시고
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 저희에게 고기를 티끌같이 내리시니 곧 바다 모래 같은 나는 새라
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 그 진중에 떨어지게 하사 그 거처에 둘리셨도다
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 저희가 먹고 배불렀나니 하나님이 저희 소욕대로 주셨도다
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 저희가 그 욕심에서 떠나지 아니하고 저희 식물이 아직 그 입에 있을 때에
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 하나님이 저희를 대하여 노를 발하사 저희 중 살진 자를 죽이시며 이스라엘의 청년을 쳐 엎드러뜨리셨도다
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 그럴지라도 저희가 오히려 범죄하여 그의 기사를 믿지 아니하였으므로
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 하나님이 저희 날을 헛되이 보내게 하시며 저희 해를 두렵게 지내게 하셨도다
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 하나님이 저희를 죽이실 때에 저희가 그에게 구하며 돌이켜 하나님을 간절히 찾았고
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 하나님이 저희의 반석이시요 지존하신 하나님이 저희 구속자이심을 기억하였도다
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 그러나 저희가 입으로 그에게 아첨하며 자기 혀로 그에게 거짓을 말하였으니
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 이는 하나님께 향하는 저희 마음이 정함이 없으며 그의 언약에 성실치 아니하였음이로다
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 오직 하나님은 자비하심으로 죄악을 사하사 멸하지 아니하시고 그 진노를 여러번 돌이키시며 그 분을 다 발하지 아니하셨으니
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 저희는 육체 뿐이라 가고 다시 오지 못하는 바람임을 기억하셨음이로다
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 저희가 광야에서 그를 반항하며 사막에서 그를 슬프시게 함이 몇번인고
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 저희가 돌이켜 하나님을 재삼 시험하며 이스라엘의 거룩한 자를 격동하였도다
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 저희가 그의 권능을 기억지 아니하며 대적에게서 구속하신 날도 생각지 아니하였도다
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 그 때에 하나님이 애굽에서 그 징조를, 소안 들에서 그 기사를 나타내사
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 저희의 강과 시내를 피로 변하여 저희로 마실수 없게 하시며
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 파리 떼를 저희 중에 보내어 물게 하시고 개구리를 보내어 해하게 하셨으며
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 저희의 토산물을 황충에게 주시며 저희의 수고한 것을 메뚜기에게 주셨으며
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 저희 포도나무를 우박으로, 저희 뽕나무를 서리로 죽이셨으며
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 저희 가축을 우박에, 저희 양떼를 번갯불에 붙이셨으며
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 그 맹렬한 노와 분과 분노와 고난 곧 벌하는 사자들을 저희에게 내려 보내셨으며
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 그 노를 위하여 치도하사 저희 혼의 사망을 면케 아니하시고 저희 생명을 염병에 붙이셨으며
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 애굽에서 모든 장자 곧 함의 장막에 있는 그 기력의 시작을 치셨으나
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 자기 백성을 양 같이 인도하여 내시고 광야에서 양떼같이 지도하셨도다
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 저희를 안전히 인도하시니 저희는 두려움이 없었으나 저희 원수는 바다에 엄몰되었도다
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 저희를 그 성소의 지경 곧 그의 오른손이 취하신 산으로 인도하시고
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 또 열방을 저희 앞에서 쫓아 내시며 줄로 저희 기업을 분배하시고 이스라엘 지파로 그 장막에 거하게 하셨도다
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 그럴지라도 저희가 지존하신 하나님을 시험하며 반항하여 그 증거를 지키지 아니하며
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 저희 열조같이 배반하고 궤사를 행하여 속이는 활 같이 빗가서
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 자기 산당으로 그 노를 격동하며 저희 조각한 우상으로 그를 진노케 하였으매
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 하나님이 들으시고 분내어 이스라엘을 크게 미워하사
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 실로의 성막 곧 인간에 세우신 장막을 떠나시고
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 그 능력된 자를 포로에 붙이시며 자기 영광을 대적의 손에 붙이시고
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 그 백성을 또 칼에 붙이사 그의 기업에게 분내셨으니
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 저희 청년은 불에 살라지고 저희 처녀에게는 혼인 노래가 없으며
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 저희 제사장들은 칼에 엎드러지고 저희 과부들은 애곡하지 못하였도다
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 때에 주께서 자다가 깬 자 같이 포도주로 인하여 외치는 용사 같이 일어나사
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 그 대적들을 쳐 물리쳐서 길이 욕되게 하시고
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 또 요셉의 장막을 싫어 버리시며 에브라임 지파를 택하지 아니하시고
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 오직 유다 지파와 그 사랑하시는 시온산을 택하시고
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 그 성소를 산의 높음 같이, 영원히 두신 땅 같이 지으셨으며
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 또 그 종 다윗을 택하시되 양의 우리에서 취하시며
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 젖 양을 지키는 중에서 저희를 이끄사 그 백성인 야곱 그 기업인 이스라엘을 기르게 하셨더니
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 이에 저가 그 마음의 성실함으로 기르고 그 손의 공교함으로 지도하였도다
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

< 시편 78 >