< 시편 7 >

1 (다윗의 식가욘. 베냐민인 구시의 말에 대하여 여호와께 한 노래) 여호와 내 하나님이여, 주께 피하오니 나를 쫓는 모든 자에게서 나를 구하여 건지소서
Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini. Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
2 건져낼 자 없으면 저희가 사자 같이 나를 찢고 뜯을까 하나이다
la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
3 여호와 내 하나님이여, 내가 이것을 행하였거나 내 손에 죄악이 있거나
Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,
4 화친한 자를 악으로 갚았거나 내 대적에게 무고히 빼앗았거든
au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
5 원수로 나의 영혼을 쫓아 잡아 내 생명을 땅에 짓밟고 내 영광을 진토에 떨어뜨리게 하소서 (셀라)
basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.
6 여호와여, 진노로 일어나사 내 대적들의 노를 막으시며 나를 위하여 깨소서 주께서 심판을 명하셨나이다
Amka kwa hasira yako, Ee Bwana, inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu. Amka, Mungu wangu, uamue haki.
7 민족들의 집회로 주를 두르게 하시고 그 위 높은 자리에 돌아오소서
Kusanyiko la watu na likuzunguke. Watawale kutoka juu.
8 여호와께서 만민에게 심판을 행하시오니 여호와여, 나의 의와 내게 있는 성실함을 따라 나를 판단하소서
Bwana na awahukumu kabila za watu. Nihukumu Ee Bwana, kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya uadilifu wangu, Ewe Uliye Juu Sana.
9 악인의 악을 끊고 의인을 세우소서 의로우신 하나님이 사람의 심장을 감찰하시나이다
Ee Mungu mwenye haki, uchunguzaye mawazo na mioyo, komesha ghasia za waovu na ufanye wenye haki waishi kwa amani.
10 나의 방패는 마음이 정직한 자를 구원하시는 하나님께 있도다
Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, awaokoaye wanyofu wa moyo.
11 하나님은 의로우신 재판장이심이여, 매일 분노하시는 하나님이시로다
Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu aghadhibikaye kila siku.
12 사람이 회개치 아니하면 저가 그 칼을 갈으심이여 그 활을 이미 당기어 예비하셨도다
Kama hakutuhurumia, atanoa upanga wake, ataupinda na kuufunga uzi upinde wake.
13 죽일 기계를 또한 예비하심이여 그 만든 살은 화전이로다
Ameandaa silaha zake kali, ameweka tayari mishale yake ya moto.
14 악인이 죄악을 해산함이여 잔해를 잉태하며 궤휼을 낳았도다
Yeye aliye na mimba ya uovu na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.
15 저가 웅덩이를 파 만듦이여 제가 만든 함정에 빠졌도다
Yeye achimbaye shimo na kulifukua hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
16 그 잔해는 자기 머리로 돌아오고 그 포학은 자기 정수리에 내리리로다
Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.
17 내가 여호와의 의를 따라 감사함이여 지극히 높으신 여호와의 이름을 찬양하리로다!
Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake, na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.

< 시편 7 >