< 시편 63 >

1 (다윗의 시. 유다 광야에 있을 때에) 하나님이여, 주는 나의 하나님이시라 내가 간절히 주를 찾되 물이 없어 마르고 곤핍한 땅에서 내 영혼이 주를 갈망하며 내 육체가 주를 앙모하나이다
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 내가 주의 권능과 영광을 보려 하여 이와 같이 성소에서 주를 바라보았나이다
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 주의 인자가 생명보다 나으므로 내 입술이 주를 찬양할 것이라
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 이러므로 내 평생에 주를 송축하며 주의 이름으로 인하여 내 손을 들리이다
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 골수와 기름진 것을 먹음과 같이 내 영혼이 만족할 것이라 내 입이 기쁜 입술로 주를 찬송하되
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 내가 나의 침상에서 주를 기억하며 밤중에 주를 묵상할 때에 하오리니
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 주는 나의 도움이 되셨음이라 내가 주의 날개 그늘에서 즐거이 부르리이다
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 나의 영혼이 주를 가까이 따르니 주의 오른손이 나를 붙드시거니와
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 나의 영혼을 찾아 멸하려 하는 저희는 땅 깊은 곳에 들어가며
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 칼의 세력에 붙인바 되어 시랑의 밥이 되리이다
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 왕은 하나님을 즐거워하리니 주로 맹세한 자마다 자랑할 것이나 거짓말 하는 자의 입은 막히리로다
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< 시편 63 >