< 시편 51 >

1 (다윗의 시. 영장으로 한 노래, 다윗이 밧세바와 동침한 후 선지자 나단이 저에게 온 때에) 하나님이여, 주의 인자를 좇아 나를 긍휼히 여기시며 주의 많은 자비를 좇아 내 죄과를 도말하소서
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba. Ee Mungu, unihurumie, kwa kadiri ya upendo wako usiokoma, kwa kadiri ya huruma yako kuu, uyafute makosa yangu.
2 나의 죄악을 말갛게 씻기시며 나의 죄를 깨끗이 제하소서
Unioshe na uovu wangu wote na unitakase dhambi yangu.
3 대저 나는 내 죄과를 아오니 내 죄가 항상 내 앞에 있나이다
Kwa maana ninajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 내가 주께만 범죄하여 주의 목전에 악을 행하였사오니 주께서 말씀하실 때에 의로우시다 하고 판단하실 때에 순전하시다 하리이다
Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 내가 죄악 중에 출생하였음이여 모친이 죄중에 나를 잉태하였나이다
Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 중심에 진실함을 주께서 원하시오니 내 속에 지혜를 알게 하시리이다
Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni, ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
7 우슬초로 나를 정결케 하소서 내가 정하리이다 나를 씻기소서 내가 눈보다 희리이다
Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi, unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 나로 즐겁고 기쁜 소리를 듣게 하사 주께서 꺾으신 뼈로 즐거워하게 하소서
Unipe kusikia furaha na shangwe, mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 주의 얼굴을 내 죄에서 돌이키시고 내 모든 죄악을 도말하소서
Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu, na uufute uovu wangu wote.
10 하나님이여, 내 속에 정한 마음을 창조하시고 내 안에 정직한 영을 새롭게 하소서
Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.
11 나를 주 앞에서 쫓아내지 마시며 주의 성신을 내게서 거두지 마소서
Usinitupe kutoka mbele zako wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.
12 주의 구원의 즐거움을 내게 회복시키시고 자원하는 심령을 주사 나를 붙드소서
Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, unipe roho ya utii, ili initegemeze.
13 그러하면 내가 범죄자에게 주의 도를 가르치리니 죄인들이 주께 돌아오리이다
Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14 하나님이여, 나의 구원의 하나님이여, 피흘린 죄에서 나를 건지소서 내 혀가 주의 의를 높이 노래하리이다
Ee Mungu, Mungu uniokoaye, niokoe na hatia ya kumwaga damu, nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako.
15 주여 내 입술을 열어 주소서 내 입이 주를 찬송하여 전파하리이다
Ee Bwana, fungua midomo yangu, na kinywa changu kitatangaza sifa zako.
16 주는 제사를 즐겨 아니하시나니 그렇지 않으면 내가 드렸을 것이라 주는 번제를 기뻐 아니하시나이다
Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta, hufurahii sadaka za kuteketezwa.
17 하나님의 구하시는 제사는 상한 심령이라 하나님이여, 상하고 통회하는 마음을 주께서 멸시치 아니하시리이다
Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika, moyo uliovunjika wenye toba, Ee Mungu, hutaudharau.
18 주의 은택으로 시온에 선을 행하시고 예루살렘 성을 쌓으소서
Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi, ukazijenge upya kuta za Yerusalemu.
19 그 때에 주께서 의로운 제사와 번제와 온전한 번제를 기뻐하시리니 저희가 수소로 주의 단에 드리리이다
Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki, sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana, pia mafahali watatolewa madhabahuni mwako.

< 시편 51 >