< 시편 48 >

1 (고라 자손의 시. 곧 노래) 여호와는 광대하시니 우리 하나님의 성, 거룩한 산에서 극진히 찬송하리로다
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 터가 높고 아름다워 온 세계가 즐거워함이여 큰 왕의 성 곧 북방에 있는 시온산이 그러하도다
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 하나님이 그 여러 궁중에서 자기를 피난처로 알리셨도다
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 열왕이 모여 함께 지났음이여
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 저희가 보고 놀라고 두려워 빨리 갔도다
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 거기서 떨림이 저희를 잡으니 고통이 해산하는 여인 같도다
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 주께서 동풍으로 다시스의 배를 깨뜨리시도다
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 우리가 들은 대로 만군의 여호와의 성, 우리 하나님의 성에서 보았나니 하나님이 이를 영영히 견고케 하시리로다 (셀라)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 하나님이여, 우리가 주의 전가운데서 주의 인자하심을 생각하였나이다
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 하나님이여, 주의 이름과 같이 찬송도 땅끝까지 미쳤으며 주의 오른손에는 정의가 충만하나이다
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 주의 판단을 인하여 시온산은 기뻐하고 유다의 딸들은 즐거워 할지어다
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 너희는 시온을 편답하고 그것을 순행하며 그 망대들을 계수하라
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 그 성벽을 자세히 보고 그 궁전을 살펴서 후대에 전하라
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 이 하나님은 영영히 우리 하나님이시니 우리를 죽을 때까지 인도하시리로다
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< 시편 48 >