< 시편 37 >

1 (다윗의 시) 행악자를 인하여 불평하여 하지 말며 불의를 행하는 자를 투기하지 말지어다
Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,
2 저희는 풀과 같이 속히 베임을 볼 것이며 푸른 채소 같이 쇠잔할 것임이로다
kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.
3 여호와를 의뢰하여 선을 행하라! 땅에 거하여 그의 성실로 식물을 삼을지어다
Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
4 또 여호와를 기뻐하라! 저가 네 마음의 소원을 이루어 주시리로다
Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
5 너의 길을 여호와께 맡기라! 저를 의지하면 저가 이루시고
Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
6 네 의를 빛같이 나타내시며 네 공의를 정오의 빛같이 하시리로다
Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
7 여호와 앞에 잠잠하고 참아 기다리라! 자기 길이 형통하며 악한 꾀를 이루는 자를 인하여 불평하여 말지어다
Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.
8 분을 그치고 노를 버리라 불평하여 말라 행악에 치우칠 뿐이라
Epuka hasira na uache ghadhabu, usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.
9 대저 행악하는 자는 끊어질 것이나 여호와를 기대하는 자는 땅을 차지하리로다
Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.
10 잠시 후에 악인이 없어지리니 네가 그곳을 자세히 살필지라도 없으리로다
Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.
11 오직 온유한 자는 땅을 차지하며 풍부한 화평으로 즐기리로다
Bali wanyenyekevu watairithi nchi na wafurahie amani tele.
12 악인이 의인 치기를 꾀하고 향하여 그 이를 가는도다
Waovu hula njama dhidi ya wenye haki na kuwasagia meno,
13 주께서 저를 웃으시리니 그 날의 이름을 보심이로다
bali Bwana huwacheka waovu, kwa sababu anajua siku yao inakuja.
14 악인이 칼을 빼고 활을 당기어 가난하고 궁핍한 자를 엎드러뜨리며 행위가 정직한 자를 죽이고자 하나
Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde, ili wawaangushe maskini na wahitaji, kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
15 그 칼은 자기의 마음을 찌르고 그 활은 부러지리로다
Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.
16 의인의 적은 소유가 많은 악인의 풍부함보다 승하도다
Bora kidogo walicho nacho wenye haki kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;
17 악인의 팔은 부러지나 의인은 여호와께서 붙드시는도다
kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
18 여호와께서 완전한 자의 날을 아시니 저희 기업은 영원하리로다
Bwana anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele.
19 저희는 환난 때에 부끄럽지 아니하며 기근의 날에도 풍족하려니와
Siku za maafa hawatanyauka, siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.
20 악인은 멸망하고 여호와의 원수는 어린 양의 기름 같이 타서 연기되어 없어지리로다
Lakini waovu wataangamia: Adui za Bwana watakuwa kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi.
21 악인은 꾸고 갚지 아니하나 의인은 은혜를 베풀고 주는도다
Waovu hukopa na hawalipi, bali wenye haki hutoa kwa ukarimu.
22 주의 복을 받은 자는 땅을 차지하고 주의 저주를 받은 자는 끊어지리로다
Wale wanaobarikiwa na Bwana watairithi nchi, bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.
23 여호와께서 사람의 걸음을 정하시고 그 길을 기뻐하시나니
Kama Bwana akipendezwa na njia ya mtu, yeye huimarisha hatua zake,
24 저는 넘어지나 아주 엎드러지지 아니함은 여호와께서 손으로 붙드심이로다
ajapojikwaa, hataanguka, kwa maana Bwana humtegemeza kwa mkono wake.
25 내가 어려서부터 늙기까지 의인이 버림을 당하거나 그 자손이 걸식함을 보지 못하였도다
Nilikuwa kijana na sasa ni mzee, lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa au watoto wao wakiombaomba chakula.
26 저는 종일토록 은혜를 베풀고 꾸어 주니 그 자손이 복을 받는도다
Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti. Watoto wao watabarikiwa.
27 악에서 떠나 선을 행하라! 그리하면 영영히 거하리니
Acha ubaya na utende wema, nawe utaishi katika nchi milele.
28 여호와께서 공의를 사랑하시고 그 성도를 버리지 아니하심이로다 저희는 영영히 보호를 받으나 악인의 자손은 끊어지리로다
Kwa kuwa Bwana huwapenda wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake. Watalindwa milele, lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali.
29 의인이 땅을 차지함이여 거기 영영히 거하리로다
Wenye haki watairithi nchi, na kuishi humo milele.
30 의인의 입은 지혜를 말하고 그 혀는 공의를 이르며
Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima, nao ulimi wake huzungumza lililo haki.
31 그 마음에는 하나님의 법이 있으니 그 걸음에 실족함이 없으리로다
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; nyayo zake hazitelezi.
32 악인이 의인을 엿보아 살해할 기회를 찾으나
Watu waovu huvizia wenye haki, wakitafuta kuwaua;
33 여호와는 저를 그 손에 버려두지 아니하시고 재판 때에도 정죄치 아니하시리로다
lakini Bwana hatawaacha mikononi mwao wala hatawaacha wahukumiwe kuwa wakosa wanaposhtakiwa.
34 여호와를 바라고 그 도를 지키라! 그리하면 너를 들어 땅을 차지하게 하실 것이라 악인이 끊어질 때에 네가 목도하리로다
Mngojee Bwana, na uishike njia yake. Naye atakutukuza uirithi nchi, waovu watakapokatiliwa mbali, utaliona hilo.
35 내가 악인의 큰 세력을 본즉 그 본토에 선 푸른 나무의 무성함 같으나
Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,
36 사람이 지날 때에 저가 없어졌으니 내가 찾아도 발견치 못하였도다
lakini alitoweka mara na hakuonekana, ingawa nilimtafuta, hakupatikana.
37 완전한 사람을 살피고 정직한 자를 볼지어다 화평한 자의 결국은 평안이로다
Watafakari watu wasio na hatia, wachunguze watu wakamilifu, kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani.
38 범죄자들은 함께 멸망하리니 악인의 결국은 끊어질 것이나
Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa, mafanikio yao yatakatiliwa mbali.
39 의인의 구원은 여호와께 있으니 그는 환난 때에 저희 산성이시로다
Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Bwana, yeye ni ngome yao wakati wa shida.
40 여호와께서 저희를 도와 건지시되 악인에게서 건져 구원하심은 그를 의지한 연고로다
Bwana huwasaidia na kuwaokoa, huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi, kwa maana wanamkimbilia.

< 시편 37 >