< 시편 18 >

1 (여호와의 종 다윗의 시. 영장으로 한 노래. 여호와께서 다윗을 그 모든 원수와 사울의 손에서 구원하신 날에 다윗이 이 노래의 말로 여호와께 아뢰어 가로되) 나의 힘이 되신 여호와여, 내가 주를 사랑하나이다
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
2 여호와는 나의 반석이시요, 나의 요새시요, 나를 건지시는 자시요, 나의 하나님이시요, 나의 피할 바위시요, 나의 방패시요, 나의 구원의 뿔이시요, 나의 산성이시로다
Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
3 내가 찬송 받으실 여호와께 아뢰리니 내 원수들에게서 구원을 얻으리로다
Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 사망의 줄이 나를 얽고 불의의 창수가 나를 두렵게 하였으며
Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
5 음부의 줄이 나를 두르고 사망의 올무가 내게 이르렀도다 (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
6 내가 환난에서 여호와께 아뢰며 나의 하나님께 부르짖었더니 저가 그 전에서 내 소리를 들으심이여 그 앞에서 나의 부르짖음이 그 귀에 들렸도다
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
7 이에 땅이 진동하고 산의 터도 요동하였으니 그의 진노를 인함이로다
Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
8 그 코에서 연기가 오르고 입에서 불이 나와 사름이여 그 불에 숯이 피었도다
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
9 저가 또 하늘을 드리우시고 강림하시니 그 발 아래는 어둑캄캄하도다
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
10 그룹을 타고 날으심이여 바람 날개로 높이 뜨셨도다
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
11 저가 흑암으로 그 숨는 곳을 삼으사 장막 같이 자기를 두르게 하심이여 곧 물의 흑암과 공중의 빽빽한 구름으로 그리하시도다
Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
12 그 앞에 광채로 인하여 빽빽한 구름이 지나며 우박과 숯불이 내리도다
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
13 여호와께서 하늘에서 뇌성을 발하시고 지존하신 자가 음성을 내시며 우박과 숯불이 내리도다
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
14 그 살을 날려 저희를 흩으심이여 많은 번개로 파하셨도다
Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
15 이럴 때에 여호와의 꾸지람과 콧김을 인하여 물밑이 드러나고 세상의 터가 나타났도다
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
16 저가 위에서 보내사 나를 취하심이여 많은 물에서 나를 건져 내셨도다
Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
17 나를 강한 원수와 미워하는 자에게서 건지셨음이여 저희는 나보다 힘센 연고로다
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
18 저희가 나의 재앙의 날에 내게 이르렀으나 여호와께서 나의 의지가 되셨도다
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
19 나를 또 넓은 곳으로 인도하시고 나를 기뻐하심으로 구원하셨도다
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
20 여호와께서 내 의를 따라 상 주시며 내 손의 깨끗함을 좇아 갚으셨으니
Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
21 이는 내가 여호와의 도를 지키고 악하게 내 하나님을 떠나지 아니 하였으며
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
22 그 모든 규례가 내 앞에 있고 내게서 그 율례를 버리지 아니하였음이로다
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
23 내가 또한 그 앞에 완전하여 나의 죄악에서 스스로 지켰나니
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
24 그러므로 여호와께서 내 의를 따라 갚으시되 그 목전에 내 손의 깨끗한대로 내게 갚으셨도다
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
25 자비한 자에게는 주의 자비하심을 나타내시며 완전한 자에게는 주의 완전하심을 보이시며
Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
26 깨끗한 자에게는 주의 깨끗하심을 보이시며 사특한 자에게는 주의 거스리심을 보이시리니
Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
27 주께서 곤고한 백성은 구원하시고 교만한 눈은 낮추시리이다
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
28 주께서 나의 등불을 켜심이여, 여호와 내 하나님이 내 흑암을 밝히시리이다
Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
29 내가 주를 의뢰하고 적군에 달리며 내 하나님을 의지하고 담을 뛰어 넘나이다
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
30 하나님의 도는 완전하고 여호와의 말씀은 정미하니 저는 자기에게 피하는 모든 자의 방패시로다
Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
31 여호와 외에 누가 하나님이며 우리 하나님 외에 누가 반석이뇨
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
32 이 하나님이 힘으로 내게 띠 띠우시며 내 길을 완전케 하시며
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
33 나의 발로 암사슴 발 같게 하시며 나를 나의 높은 곳에 세우시며
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
34 내 손을 가르쳐 싸우게 하시니 내 팔이 놋 활을 당기도다
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
35 주께서 또 주의 구원하는 방패를 내게 주시며 주의 오른손이 나를 붙들고 주의 온유함이 나를 크게 하셨나이다
Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
36 내 걸음을 넓게 하셨고 나로 실족지 않게 하셨나이다
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
37 내가 내 원수를 따라 미치리니 저희가 망하기 전에는 돌이키지 아니하리이다
Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
38 내가 저희를 쳐서 능히 일어나지 못하게 하리니 저희가 내 발 아래 엎드러지리이다
Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
39 대저 주께서 나로 전쟁케 하려고 능력으로 내게 띠 띠우사 일어나 나를 치는 자로 내게 굴복케 하셨나이다
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
40 주께서 또 내 원수들로 등을 내게로 향하게 하시고 나로 나를 미워 하는 자를 끊어버리게 하셨나이다
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
41 저희가 부르짖으나 구원할 자가 없었고 여호와께 부르짖어도 대답지 아니하셨나이다
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
42 내가 저희를 바람 앞에 티끌 같이 부숴뜨리고 거리의 진흙 같이 쏟아 버렸나이다
Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
43 주께서 나를 백성의 다툼에서 건지시고 열방의 으뜸을 삼으셨으니 내가 알지 못하는 백성이 나를 섬기리이다
Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
44 저희가 내 풍성을 들은 즉시로 내게 순복함이여 이방인들이 내게 복종하리로다
Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
45 이방인들이 쇠미하여 그 견고한 곳에서 떨며 나오리로다
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
46 여호와는 생존하시니 나의 반석을 찬송하며 내 구원의 하나님을 높일지로다
Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
47 이 하나님이 나를 위하여 보수하시고 민족들로 내게 복종케 하시도다
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
48 주께서 나를 내 원수들에게서 구조하시니 주께서 실로 나를 대적하는 자의 위에 나를 드시고 나를 강포한 자에게서 건지시나이다
aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
49 여호와여, 이러므로 내가 열방 중에서 주께 감사하며 주의 이름을 찬송하리이다
Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
50 여호와께서 그 왕에게 큰 구원을 주시며 기름 부음 받은 자에게 인자를 베푸심이여 영영토록 다윗과 그 후손에게로다
Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.

< 시편 18 >