< 시편 139 >

1 (다윗의 시. 영장으로 한 노래) 여호와여, 주께서 나를 감찰하시고 아셨나이다
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
2 주께서 나의 앉고 일어섬을 아시며 멀리서도 나의 생각을 통촉하시오며
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3 나의 길과 눕는 것을 감찰하시며 나의 모든 행위를 익히 아시오니
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
4 여호와여, 내 혀의 말을 알지 못하시는 것이 하나도 없으시니이다
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
5 주께서 나의 전후를 두르시며 내게 안수하셨나이다
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
6 이 지식이 내게 너무 기이하니 높아서 내가 능히 미치지 못하나이다
Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
7 내가 주의 신을 떠나 어디로 가며 주의 앞에서 어디로 피하리이까
Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
8 내가 하늘에 올라갈지라도 거기 계시며 음부에 내 자리를 펼지라도 거기 계시니이다 (Sheol h7585)
Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol h7585)
9 내가 새벽 날개를 치며 바다 끝에 가서 거할지라도
Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
10 곧 거기서도 주의 손이 나를 인도하시며 주의 오른손이 나를 붙드시리이다
hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
11 내가 혹시 말하기를 흑암이 정녕 나를 덮고 나를 두른 빛은 밤이 되리라 할지라도
Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
12 주에게서는 흑암이 숨기지 못하며 밤이 낮과 같이 비취나니 주에게는 흑암과 빛이 일반이니이다
hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
13 주께서 내 장부를 지으시며 나의 모태에서 나를 조직하셨나이다
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
14 내가 주께 감사하옴은 나를 지으심이 신묘막측하심이라 주의 행사가 기이함을 내 영혼이 잘 아나이다
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
15 내가 은밀한 데서 지음을 받고 땅의 깊은 곳에서 기이하게 지음을 받은 때에 나의 형체가 주의 앞에 숨기우지 못하였나이다
Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
16 내 형질이 이루기 전에 주의 눈이 보셨으며 나를 위하여 정한 날이 하나도 되기 전에 주의 책에 다 기록이 되었나이다
macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
17 하나님이여, 주의 생각이 내게 어찌 그리 보배로우신지요 그 수가 어찌 그리 많은지요
Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
18 내가 세려고 할지라도 그 수가 모래보다 많도소이다 내가 깰 때에도 오히려 주와 함께 있나이다
Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
19 하나님이여, 주께서 정녕히 악인을 죽이시리이다 피흘리기를 즐기는 자들아 나를 떠날지어다
Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
20 저희가 주를 대하여 악하게 말하며 주의 원수들이 헛되이 주의 이름을 칭하나이다
Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
21 여호와여, 내가 주를 미워하는 자를 미워하지 아니하오며 주를 치러 일어나는 자를 한하지 아니하나이까
Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
22 내가 저희를 심히 미워하니 저희는 나의 원수니이다
Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
23 하나님이여, 나를 살피사 내 마음을 아시며 나를 시험하사 내 뜻을 아옵소서
Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
24 내게 무슨 악한 행위가 있나 보시고 나를 영원한 길로 인도하소서
Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.

< 시편 139 >