< 시편 135 >

1 할렐루야 여호와의 이름을 찬송하라! 여호와의 종들아 찬송하라!
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 여호와의 집 우리 하나님의 전정에 섰는 너희여,
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 여호와를 찬송하라! 여호와는 선하시며 그 이름이 아름다우니 그 이름을 찬양하라!
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 여호와께서 자기를 위하여 야곱 곧 이스라엘을 자기의 특별한 소유로 택하셨음이로다
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 내가 알거니와 여호와께서는 광대하시며 우리 모든 신보다 높으시도다
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 여호와께서 무릇 기뻐하시는 일을 천지와 바다와 모든 깊은 데서 행하셨도다
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 안개를 땅 끝에서 일으키시며 비를 위하여 번개를 만드시며 바람을 그 곳간에서 내시는도다
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 저가 애굽의 처음 난 자를 사람부터 짐승까지 치셨도다
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 애굽이여, 여호와께서 너의 중에 징조와 기사를 보내사 바로와 그 모든 신복에게 임하게 하셨도다
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 저가 많은 나라를 치시고 강한 왕들을 죽이셨나니
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 곧 아모리인의 왕 시혼과 바산 왕 옥과 가나안의 모든 국왕이로다
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 저희의 땅을 기업으로 주시되 자기 백성 이스라엘에게 기업으로 주셨도다
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 여호와여, 주의 이름이 영원하시니이다 여호와여, 주의 기념이 대대에 이르리이다
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 여호와께서 자기 백성을 판단하시며 그 종들을 긍휼히 여기시리로다
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 열방의 우상은 은, 금이요 사람의 수공물이라
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 입이 있어도 말하지 못하며 눈이 있어도 보지 못하며
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 귀가 있어도 듣지 못하며 그 입에는 아무 기식도 없나니
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 그것을 만든자와 그것을 의지하는 자가 다 그것과 같으리라
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 이스라엘 족속아 여호와를 송축하라! 아론의 족속아 여호와를 송축하라!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 레위 족속아 여호와를 송축하라! 여호와를 경외하는 너희들아 여호와를 송축하라!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 예루살렘에 거하신 여호와는 시온에서 찬송을 받으실지어다! 할렐루야
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< 시편 135 >