< 시편 118 >

1 여호와께 감사하라! 저는 선하시며 그 인자하심이 영원함이로다
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 이제 이스라엘은 말하기를 그 인자하심이 영원하다 할지로다
Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
3 이제 아론의 집은 말하기를 그 인자하심이 영원하다 할지로다
Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
4 이제 여호와를 경외하는 자는 말하기를 그 인자하심이 영원하다 할지로다
Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
5 내가 고통 중에 여호와께 부르짖었더니 여호와께서 답하시고 나를 광활한 곳에 세우셨도다
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 여호와는 내 편이시라 내게 두려움이 없나니 내게 어찌할꼬
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 여호와께서 내 편이 되사 나를 돕는 자 중에 계시니 그러므로 나를 미워하는 자에게 보응하시는 것을 내가 보리로다
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8 여호와께 피함이 사람을 신뢰함보다 나으며
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 여호와께 피함이 방백들을 신뢰함보다 낫도다
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.

< 시편 118 >