< 시편 113 >

1 할렐루야! 여호와의 종들아 찬양하라! 여호와의 이름을 찬양하라
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 이제부터 영원까지 여호와의 이름을 찬송할지로다
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 해 돋는 데서부터 해 지는 데까지 여호와의 이름이 찬양을 받으시리로다
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 여호와는 모든 나라 위에 높으시며 그 영광은 하늘 위에 높으시도다
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 여호와 우리 하나님과 같은 자 누구리요 높은 위에 앉으셨으나
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 스스로 낮추사 천지를 살피시고
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 가난한 자를 진토에서 일으키시며 궁핍한 자를 거름 무더기에서 드셔서
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 방백들 곧 그 백성의 방백들과 함께 세우시며
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 또 잉태하지 못하던 여자로 집에 거하게 하사 자녀의 즐거운 어미가 되게 하시는도다 할렐루야
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< 시편 113 >