< 시편 109 >

1 (다윗의 시. 영장으로 한 노래) 나의 찬송하는 하나님이여, 잠잠하지 마옵소서
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 대저 저희가 악한 입과 궤사한 입을 열어 나를 치며 거짓된 혀로 내게 말하며
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 또 미워하는 말로 나를 두르고 무고히 나를 공격하였나이다
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 나는 사랑하나 저희는 도리어 나를 대적하니 나는 기도할 뿐이라
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 저희가 악으로 나의 선을 갚으며 미워함으로 나의 사랑을 갚았사오니
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 악인으로 저를 제어하게 하시며 대적으로 그 오른편에 서게 하소서
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 저가 판단을 받을 때에 죄를 지고 나오게 하시며 그 기도가 죄로 변케 하시며
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 그 년수를 단촉케 하시며 그 직분을 타인이 취하게 하시며
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 그 자녀는 고아가 되고 그 아내는 과부가 되며
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 그 자녀가 유리 구걸하며 그 황폐한 집을 떠나 빌어먹게 하소서
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 고리대금하는 자로 저의 소유를 다 취하게 하시며 저의 수고한 것을 외인이 탈취하게 하시며
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 저에게 은혜를 계속할 자가 없게 하시며 그 고아를 연휼할 자도 없게 하시며
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 그 후사가 끊어지게 하시며 후대에 저희 이름이 도말되게 하소서
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 여호와는 그 열조의 죄악을 기억하시며 그 어미의 죄를 도말하지마시고
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 그 죄악을 항상 여호와 앞에 있게 하사 저희 기념을 땅에서 끊으소서
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 저가 긍휼히 여길 일을 생각지 아니하고 가난하고 궁핍한 자와 마음이 상한 자를 핍박하여 죽이려 한 연고니이다
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 저가 저주하기를 좋아하더니 그것이 자기에게 임하고 축복하기를 기뻐 아니하더니 복이 저를 멀리 떠났으며
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 또 저주하기를 옷 입듯하더니 저주가 물같이 그 내부에 들어가며 기름 같이 그 뼈에 들어갔나이다
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 저주가 그 입는 옷 같고 항상 띠는 띠와 같게 하소서
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 이는 대적 곧 내 영혼을 대적하여 악담하는 자가 여호와께 받는 보응이니이다
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 주 여호와여, 주의 이름을 인하여 나를 선대하시며 주의 인자하심이 선함을 인하여 나를 건지소서
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 나는 가난하고 궁핍하여 중심이 상함이니이다
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 나의 가는 것은 석양 그림자 같고 또 메뚜기 같이 불려가오며
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 금식함을 인하여 내 무릎은 약하고 내 육체는 수척하오며
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 나는 또 저희의 훼방거리라 저희가 나를 본즉 머리를 흔드나이다
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 여호와 나의 하나님이여, 나를 도우시며 주의 인자하심을 좇아 나를 구원하소서
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 이것이 주의 손인 줄을 저희로 알게 하소서 여호와께서 이를 행하셨나이다
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 저희는 저주하여도 주는 내게 복을 주소서! 저희는 일어날 때에 수치를 당할지라도 주의 종은 즐거워하리이다
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 나의 대적으로 욕을 옷입듯하게 하시며 자기 수치를 겉옷 같이 입게 하소서
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 내가 입으로 여호와께 크게 감사하며 무리 중에서 찬송하리니
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 저가 궁핍한 자의 우편에 서사 그 영혼을 판단하려 하는 자에게 구원하실 것임이로다
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< 시편 109 >