< 잠언 1 >
1 다윗의 아들 이스라엘 왕 솔로몬의 잠언이라
Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 이는 지혜와 훈계를 알게 하며 명철의 말씀을 깨닫게 하며
Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 지혜롭게, 의롭게, 공평하게, 정직하게, 행할 일에 대하여 훈계를 받게 하며
ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 어리석은 자로 슬기롭게 하며 젊은 자에게 지식과 근신함을 주기 위한 것이니
Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 지혜있는 자는 듣고 학식이 더할 것이요 명철한 자는 모략을 얻을 것이라
Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
6 잠언과 비유와 지혜있는 자의 말과 그 오묘한 말을 깨달으리라
kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
7 여호와를 경외하는 것이 지식의 근본이어늘 미련한 자는 지혜와 훈계를 멸시하느니라
Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
8 내 아들아 네 아비의 훈계를 들으며 네 어미의 법을 떠나지 말라
Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9 이는 네 머리의 아름다운 관이요 네 목의 금사슬이니라
zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10 내 아들아 악한 자가 너를 꾈지라도 좇지 말라 내 아들아 악한 자가 너를 꾈지라도 좇지 말라
Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11 그들이 네게 말하기를 우리와 함께 가자 우리가 가만히 엎드렸다가 사람의 피를 흘리자 죄없는 자를 까닭없이 숨어 기다리다가
Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12 음부 같이 그들을 산 채로 삼키며 무덤에 내려가는 자 같게 통으로 삼키자 (Sheol )
Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni. (Sheol )
13 우리가 온갖 보화를 얻으며 빼앗은 것으로 우리 집에 채우리니
Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
14 너는 우리와 함께 제비를 뽑고 우리가 함께 전대 하나만 두자 할지라도
Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
15 내 아들아 그들과 함께 길에 다니지 말라 네 발을 금하여 그 길을 밟지 말라
Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;
16 대저 그 발은 악으로 달려가며 피를 흘리는 데 빠름이니라
miguu ya hukimbilia mabaya na huharakisha kumwaga damu.
17 무릇 새가 그물 치는 것을 보면 헛 일이겠거늘
Kwa kuwa haina maana kumtegea ndege mtego wakati ndege anaona.
18 그들의 가만히 엎드림은 자기의 피를 흘릴 뿐이요 숨어 기다림은 자기의 생명을 해할 뿐이니
Watu hawa huvizia kujiua wenyewe—wanatega mtego kwa ajili yao wenyewe.
19 무릇 이를 탐하는 자의 길은 다 이러하여 자기의 생명을 잃게 하느니라
Ndivyo zilivyo njia za kila ambaye hupata utajiri kwa udhalimu; mapato ya udhalimu huondoa uhai wa wenye utajiri.
20 지혜가 길거리에서 부르며 광장에서 소리를 높이며
Hekima inalia kwa sauti mtaani, inapaza sauti katika viwanja;
21 훤화하는 길 머리에서 소리를 지르며 성문 어귀와 성중에서 그 소리를 발하여 가로되
katika mitaa inalia kwa sauti kuu, kwenye maingilio ya milango ya mji inasema “
22 너희 어리석은 자들은 어리석음을 좋아하며 거만한 자들은 거만을 기뻐하며 미련한 자들은 지식을 미워하니 어느 때까지 하겠느냐
Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
23 나의 책망을 듣고 돌이키라 보라 내가 나의 신을 너희에게 부어주며 나의 말을 너희에게 보이리라
Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
24 내가 부를지라도 너희가 듣기 싫어 하였고 내가 손을 펼지라도 돌아보는 자가 없었고
Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
25 도리어 나의 모든 교훈을 멸시하며 나의 책망을 받지 아니하였은즉
Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
26 너희가 재앙을 만날 때에 내가 웃을 것이며 너희에게 두려움이 임할 때에 내가 비웃으리라
Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
27 너희의 두려움이 광풍같이 임하겠고 너희의 재앙이 폭풍같이 임하리니
hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
28 그 때에 너희가 나를 부르리라 그래도 내가 대답지 아니하겠고 부지런히 나를 찾으리라 그래도 나를 만나지 못하리니
Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
29 대저 너희가 지식을 미워하며 여호와 경외하기를 즐거워하지 아니하며
Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,
30 나의 교훈을 받지 아니하고 나의 모든 책망을 업신여겼음이라
hawakufuata mafundisho yangu na wakayadharau masahihisho yangu yote.
31 그러므로 자기 행위의 열매를 먹으며 자기 꾀에 배부르리라
Watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa kwa matunda ya hila zao wenyewe.
32 어리석은 자의 퇴보는 자기를 죽이며 미련한 자의 안일은 자기를 멸망시키려니와
kwa maana wajinga hufa wanaporudi nyuma, na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.
33 오직 나를 듣는 자는 안연히 살며 재앙의 두려움이 없이 평안하리라
Bali kila anisikilizaye ataishi kwa usalama na atapumzika salama pasipo hofu ya maafa.