< 잠언 8 >

1 지혜가 부르지 아니하느냐 명철이 소리를 높이지 아니하느냐
Je, hekima haitani? Je, ufahamu hapazi sauti?
2 그가 길가의 높은 곳과 사거리에 서며
Juu ya miinuko karibu na njia, penye njia panda, ndipo asimamapo;
3 성문 곁과 문 어귀와 여러 출입하는 문에서 불러 가로되
kando ya malango yaelekeayo mjini, kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:
4 사람들아 내가 너희를 부르며 내가 인자들에게 소리를 높이노라
“Ni ninyi wanaume, ninaowaita; ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.
5 어리석은 자들아 너희는 명철할지니라 미련한 자들아 너희는 마음이 밝을지니라 너희는 들을지어다
Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
6 내가 가장 선한 것을 말하리라 내 입술을 열어 정직을 내리라
Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
7 내 입은 진리를 말하며 내 입술은 악을 미워하느니라
Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.
8 내 입의 말은 다 의로운즉 그 가운데 굽은 것과 패역한 것이 없나니
Maneno yote ya kinywa changu ni haki; hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.
9 이는 다 총명 있는 자의 밝히 아는 바요 지식 얻은 자의 정직히 여기는 바니라
Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.
10 너희가 은을 받지 말고 나의 훈계를 받으며 정금보다 지식을 얻으라
Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, maarifa badala ya dhahabu safi,
11 대저 지혜는 진주보다 나으므로 무릇 원하는 것을 이에 비교할 수 없음이니라
kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.
12 나 지혜는 명철로 주소를 삼으며 지식과 근신을 찾아 얻나니
“Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; ninamiliki maarifa na busara.
13 여호와를 경외하는 것은 악을 미워하는 것이라 나는 교만과 거만과 악한 행실과 패역한 입을 미워하느니라
Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
14 내게는 도략과 참 지식이 있으며 나는 명철이라 내게 능력이 있으므로
Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu; nina ufahamu na nina nguvu.
15 나로 말미암아 왕들이 치리하며 방백들이 공의를 세우며
Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,
16 나로 말미암아 재상과 존귀한 자 곧 세상의 모든 재판관들이 다스리느니라
kwa msaada wangu wakuu hutawala, na wenye vyeo wote watawalao dunia.
17 나를 사랑하는 자들이 나의 사랑을 입으며 나를 간절히 찾는 자가 나를 만날 것이니라
Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
18 부귀가 내게 있고 장구한 재물과 의도 그러하니라
Utajiri na heshima viko kwangu, utajiri udumuo na mafanikio.
19 내 열매는 금이나 정금보다 나으며 내 소득은 천은보다 나으니라
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
20 나는 의로운 길로 행하며 공평한 길 가운데로 다니나니
Natembea katika njia ya unyofu katika mapito ya haki,
21 이는 나를 사랑하는 자로 재물을 얻어서 그 곳간에 채우게 하려함이니라
nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.
22 여호와께서 그 조화의 시작 곧 태초에 일하시기 전에 나를 가지셨으며
“Bwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake, kabla ya matendo yake ya zamani;
23 만세 전부터 상고부터, 땅이 생기기 전부터, 내가 세움을 입었나니
niliteuliwa tangu milele, tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa.
24 아직 바다가 생기지 아니하였고 큰 샘들이 있기 전에 내가 이미났으며
Wakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa, wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji;
25 산이 세우심을 입기 전에 언덕이 생기기 전에 내가 이미 났으니
kabla milima haijawekwa mahali pake, kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa,
26 하나님이 아직 땅도 들도 세상 진토의 근원도 짓지 아니하셨을 때에라
kabla hajaumba dunia wala mashamba yake au vumbi lolote la dunia.
27 그가 하늘을 지으시며 궁창으로 해면에 두르실 때에 내가 거기 있었고
Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, wakati alichora mstari wa upeo wa macho juu ya uso wa kilindi,
28 그가 위로 구름 하늘을 견고하게 하시며 바다의 샘들을 힘 있게하시며
wakati aliweka mawingu juu na kuziweka imara chemchemi za bahari,
29 바다의 한계를 정하여 물로 명령을 거스리지 못하게 하시며 또 땅의 기초를 정하실 때에
wakati aliiwekea bahari mpaka wake ili maji yasivunje agizo lake, na wakati aliweka misingi ya dunia.
30 내가 그 곁에 있어서 창조자가 되어 날마다 그 기뻐하신 바가 되었으며 항상 그 앞에서 즐거워하였으며
Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake. Nilijazwa na furaha siku baada ya siku, nikifurahi daima mbele zake,
31 사람이 거처할 땅에서 즐거워하며 인자들을 기뻐하였었느니라
nikifurahi katika dunia yake yote nami nikiwafurahia wanadamu.
32 아들들아 이제 내게 들으라 내 도를 지키는 자가 복이 있느니라
“Basi sasa wanangu, nisikilizeni; heri wale wanaozishika njia zangu.
33 훈계를 들어서 지혜를 얻으라 그것을 버리지 말라
Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima; msiyapuuze.
34 누구든지 내게 들으며 날마다 내 문 곁에서 기다리며 문설주 옆에서 기다리는 자는 복이 있나니
Heri mtu yule anisikilizaye mimi, akisubiri siku zote malangoni mwangu, akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu.
35 대저 나를 얻는 자는 생명을 얻고 여호와께 은총을 얻을 것임이니라
Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana.
36 그러나 나를 잃는 자는 자기의 영혼을 해하는 자라 무릇 나를 미워하는 자는 사망을 사랑하느니라
Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”

< 잠언 8 >