< 잠언 31 >

1 르무엘왕의 말씀한바 곧 그 어머니가 그를 훈계한 잠언이라
Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
2 내 아들아 내가 무엇을 말할꼬 내 태에서 난 아들아 내가 무엇을 말할꼬 서원대로 얻은 아들아 내가 무엇을 말할꼬
“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
3 네 힘을 여자들에게 쓰지 말며 왕들을 멸망시키는 일을 행치 말지어다
Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
4 르무엘아 포도주를 마시는 것이 왕에게 마땅치 아니하고 왕에게 마땅치 아니하며 독주를 찾는 것이 주권자에게 마땅치 않도다
“Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
5 술을 마시다가 법을 잊어버리고 모든 간곤한 백성에게 공의를 굽게 할까 두려우니라
wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
6 독주는 죽게된 자에게, 포도주는 마음에 근심하는 자에게 줄지어다
Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
7 그는 마시고 빈궁한 것을 잊어버리겠고 다시 그 고통을 기억지 아니하리라
Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
8 너는 벙어리와 고독한 자의 송사를 위하여 입을 열지니라
“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
9 너는 입을 열어 공의로 재판하여 간곤한 자와 궁핍한 자를 신원할지니라
Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
10 누가 현숙한 여인을 찾아 얻겠느냐 그 값은 진주보다 더 하니라
Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
11 그런 자의 남편의 마음은 그를 믿나니 산업이 핍절치 아니하겠으며
Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
12 그런 자는 살아 있는 동안에 그 남편에게 선을 행하고 악을 행치아니하느니라
Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
13 그는 양털과 삼을 구하여 부지런히 손으로 일하며
Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
14 상고의 배와 같아서 먼 데서 양식을 가져오며
Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
15 밤이 새기 전에 일어나서 그 집 사람에게 식물을 나눠주며 여종에게 일을 정하여 맡기며
Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
16 밭을 간품하여 사며 그 손으로 번 것을 가지고 포도원을 심으며
Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
17 힘으로 허리를 묶으며 그 팔을 강하게 하며
Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
18 자기의 무역하는 것이 이로운 줄을 깨닫고 밤에 등불을 끄지 아니하고
Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
19 손으로 솜뭉치를 들고 손가락으로 가락을 잡으며
Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
20 그는 간곤한 자에게 손을 펴며 궁핍한 자를 위하여 손을 내밀며
Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
21 그 집 사람들은 다 홍색 옷을 입었으므로 눈이 와도 그는 집 사람을 위하여 두려워하지 아니하며
Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
22 그는 자기를 위하여 아름다운 방석을 지으며 세마포와 자색 옷을 입으며
Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
23 그 남편은 그 땅의 장로로 더불어 성문에 앉으며 사람의 아는 바가 되며
Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
24 그는 베로 옷을 지어 팔며 띠를 만들어 상고에게 맡기며
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
25 능력과 존귀로 옷을 삼고 후일을 웃으며
Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
26 입을 열어 지혜를 베풀며 그 혀로 인애의 법을 말하며
Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
27 그 집안 일을 보살피고 게을리 얻은 양식을 먹지 아니하나니
Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
28 그 자식들은 일어나 사례하며 그 남편은 칭찬하기를
Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
29 덕행 있는 여자가 많으나 그대는 여러 여자보다 뛰어난다 하느니라
“Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 고운 것도 거짓되고 아름다운 것도 헛되나 오직 여호와를 경외하는 여자는 칭찬을 받을 것이라
Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
31 그 손의 열매가 그에게로 돌아갈 것이요 그 행한 일을 인하여 성문에서 칭찬을 받으리라
Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.

< 잠언 31 >