< 잠언 3 >

1 내 아들아 나의 법을 잊어버리지 말고 네 마음으로 나의 명령을 지키라
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 그리하면 그것이 너로 장수하여 많은 해를 누리게 하며 평강을 더하게 하리라
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3 인자와 진리로 네게서 떠나지 않게 하고 그것을 네 목에 매며 네 마음판에 새기라
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4 그리하면 네가 하나님과 사람 앞에서 은총과 귀중히 여김을 받으리라
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5 너는 마음을 다하여 여호와를 의뢰하고 네 명철을 의지하지 말라
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 너는 범사에 그를 인정하라! 그리하면 네 길을 지도하시리라
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7 스스로 지혜롭게 여기지 말지어다 여호와를 경외하며 악을 떠날지어다
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8 이것이 네 몸에 양약이 되어 네 골수로 윤택하게 하리라
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9 네 재물과 네 소산물의 처음 익은 열매로 여호와를 공경하라
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10 그리하면 네 창고가 가득히 차고 네 즙틀에 새 포도즙이 넘치리라
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11 내 아들아 여호와의 징계를 경히 여기지 말라 그 꾸지람을 싫어하지 말라
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12 대저 여호와께서 그 사랑하시는 자를 징계하시기를 마치 아비가 그 기뻐하는 아들을 징계함 같이 하시느니라
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13 지혜를 얻은 자와 명철을 얻은 자는 복이 있나니
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14 이는 지혜를 얻는 것이 은을 얻는 것보다 낫고 그 이익이 정금보다 나음이니라
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15 지혜는 진주보다 귀하니 너의 사모하는 모든 것으로 이에 비교할수 없도다
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16 그 우편 손에는 장수가 있고, 그 좌편 손에는 부귀가 있나니
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17 그 길은 즐거운 길이요 그 첩경은 다 평강이니라
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18 지혜는 그 얻은 자에게 생명나무라 지혜를 가진 자는 복되도다
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19 여호와께서는 지혜로 땅을 세우셨으며 명철로 하늘을 굳게 펴셨고
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20 그 지식으로 해양이 갈라지게 하셨으며 공중에서 이슬이 내리게 하셨느니라
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21 내 아들아 완전한 지혜와 근신을 지키고 이것들로 네 눈 앞에서 떠나지 않게 하라
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22 그리하면 그것이 네 영혼의 생명이 되며 네 목에 장식이 되리니
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23 네가 네 길을 안연히 행하겠고 네 발이 거치지 아니하겠으며
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24 네가 누울 때에 두려워하지 아니하겠고 네가 누운즉 네 잠이 달리로다
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25 너는 창졸간의 두려움이나 악인의 멸망이 임할 때나 두려워하지말라
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26 대저 여호와는 너의 의지할 자이시라 네 발을 지켜 걸리지 않게 하시리라
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27 네 손이 선을 베풀 힘이 있거든 마땅히 받을 자에게 베풀기를 아끼지 말며
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28 네게 있거든 이웃에게 이르기를 갔다가 다시 오라 내일 주겠노라 하지 말며
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29 네 이웃이 네 곁에서 안연히 살거든 그를 모해하지 말며
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30 사람이 네게 악을 행하지 아니하였거든 까닭없이 더불어 다투지말며
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31 포학한 자를 부러워하지 말며 그 아무 행위든지 좇지 말라
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32 대저 패역한 자는 여호와의 미워하심을 입거니와 정직한 자에게는 그의 교통하심이 있으며
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33 악인의 집에는 여호와의 저주가 있거니와 의인의 집에는 복이 있느니라
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34 진실로 그는 거만한 자를 비웃으시며 겸손한 자에게 은혜를 베푸시나니
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35 지혜로운 자는 영광을 기업으로 받거니와 미련한 자의 현달함은 욕이 되느니라
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.

< 잠언 3 >