< 잠언 2 >

1 내 아들아 네가 만일 나의 말을 받으며 나의 계명을 네게 간직하며
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 네 귀를 지혜에 기울이며 네 마음을 명철에 두며
kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 지식을 불러 구하며 명철을 얻으려고 소리를 높이며
na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
4 은을 구하는 것 같이 그것을 구하며 감추인 보배를 찾는 것 같이 그것을 찾으면
na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 여호와 경외하기를 깨달으며 하나님을 알게 되리니
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
6 대저 여호와는 지혜를 주시며 지식과 명철을 그 입에서 내심이며
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 그는 정직한 자를 위하여 완전한 지혜를 예비하시며 행실이 온전한 자에게 방패가 되시나니
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 대저 그는 공평의 길을 보호하시며 그 성도들의 길을 보전하려 하심이니라
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9 그런즉 네가 공의와 공평과 정직 곧 모든 선한 길을 깨달을 것이라
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
10 곧 지혜가 네 마음에 들어가며 지식이 네 영혼에 즐겁게 될 것이요
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11 근신이 너를 지키며 명철이 너를 보호하여
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
12 악한 자의 길과 패역을 말하는 자에게서 건져내리라
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
13 이 무리는 정직한 길을 떠나 어두운 길로 행하며
wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
14 행악하기를 기뻐하며 악인의 패역을 즐거워하나니
wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
15 그 길은 구부러지고 그 행위는 패역하리라
ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
16 지혜가 또 너를 음녀에게서, 말로 호리는 이방 계집에게서 구원하리니
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
17 그는 소시의 짝을 버리며 그 하나님의 언약을 잊어버린자라
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
18 그 집은 사망으로, 그 길은 음부로 기울어졌나니
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
19 누구든지 그에게로 가는 자는 돌아오지 못하며 또 생명길을 얻지 못하느니라
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
20 지혜가 너로 선한 자의 길로 행하게 하며 또 의인의 길을 지키게 하리니
Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
21 대저 정직한 자는 땅에 거하며 완전한 자는 땅에 남아 있으리라
Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
22 그러나 악인은 땅에서 끊어지겠고 궤휼한 자는 땅에서 뽑히리라
Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

< 잠언 2 >