< 잠언 18 >

1 무리에게서 스스로 나뉘는 자는 자기 소욕을 따르는 자라 온갖 참 지혜를 배척하느니라
Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.
2 미련한 자는 명철을 기뻐하지 아니하고 자기의 의사를 드러내기만 기뻐하느니라
Mpumbavu hafurahii ufahamu, bali hufurahia kutangaza maoni yake mwenyewe.
3 악한 자가 이를 때에는 멸시도 따라오고 부끄러운 것이 이를 때에는 능욕도 함께 오느니라
Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia, pamoja na aibu huja lawama.
4 명철한 사람의 입의 말은 깊은 물과 같고 지혜의 샘은 솟쳐 흐르는 내와 같으니라
Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji, bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
5 악인을 두호하는 것과 재판할 때에 의인을 억울하게 하는 것이 선하지 아니하니라
Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.
6 미련한 자의 입술은 다툼을 일으키고 그 입은 매를 자청하느니라
Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.
7 미련한 자의 입은 그의 멸망이 되고 그 입술은 그의 영혼의 그물이 되느니라
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.
8 남의 말하기를 좋아하는 자의 말은 별식과 같아서 뱃 속 깊은 데로 내려가느니라
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
9 자기의 일을 게을리 하는 자는 패가 하는 자의 형제니라
Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.
10 여호와의 이름은 견고한 망대라 의인은 그리로 달려가서 안전함을 얻느니라
Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
11 부자의 재물은 그의 견고한 성이라 그가 높은 성벽 같이 여기느니라
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.
12 사람의 마음의 교만은 멸망의 선봉이요 겸손은 존귀의 앞잡이니라
Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima.
13 사연을 듣기 전에 대답하는 자는 미련하여 욕을 당하느니라
Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake.
14 사람의 심령은 그 병을 능히 이기려니와 심령이 상하면 그것을 누가 일으키겠느냐
Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?
15 명철한 자의 마음은 지식을 얻고 지혜로운 자의 귀는 지식을 구하느니라
Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.
16 선물은 그 사람의 길을 너그럽게 하며 또 존귀한 자의 앞으로 그를 인도하느니라
Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.
17 송사에 원고의 말이 바른 것 같으나 그 피고가 와서 밝히느니라
Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi, hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.
18 제비 뽑는 것은 다툼을 그치게 하여 강한 자 사이에 해결케 하느니라
Kupiga kura hukomesha mashindano na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.
19 노엽게 한 형제와 화목하기가 견고한 성을 취하기 보다 어려운즉 이러한 다툼은 산성 문빗장 같으니라
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.
20 사람은 입에서 나오는 열매로 하여 배가 부르게 되나니 곧 그 입술에서 나는 것으로하여 만족케 되느니라
Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake, atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.
21 죽고 사는 것이 혀의 권세에 달렸나니 혀를 쓰기 좋아하는 자는 그 열매를 먹으리라
Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi, nao waupendao watakula matunda yake.
22 아내를 얻는 자는 복을 얻고 여호와께 은총을 받는 자니라
Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa Bwana.
23 가난한 자는 간절한 말로 구하여도 부자는 엄한 말로 대답하느니라
Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.
24 많은 친구를 얻는 자는 해를 당하게 되거니와 어떤 친구는 형제보다 친밀하니라
Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu, bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.

< 잠언 18 >