< 욥기 8 >

1 수아 사람 빌닷이 대답하여 가로되
Kisha Bildadi Mshuhi akajibu:
2 네가 어느 때까지 이런 말을 하겠으며 어느 때까지 네 입의 말이 광풍과 같겠는가
“Hata lini wewe utasema mambo kama haya? Maneno yako ni kama upepo mkuu.
3 하나님이 어찌 심판을 굽게 하시겠으며 전능하신이가 어찌 공의를 굽게 하시겠는가
Je, Mungu hupotosha hukumu? Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?
4 네 자녀들이 주께 득죄하였으므로 주께서 그들을 그 죄에 붙이셨나니
Watoto wako walipomtenda dhambi, aliwapa adhabu ya dhambi yao.
5 네가 만일 하나님을 부지런히 구하며 전능하신 이에게 빌고
Lakini ukimtafuta Mungu, nawe ukamsihi Mwenyezi,
6 또 청결하고 정직하면 정녕 너를 돌아보시고 네 의로운 집으로 형통하게 하실 것이라
ikiwa wewe ni safi na mnyofu, hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako, na kukurudisha katika mahali pako pa haki.
7 네 시작은 미약하였으나 네 나중은 심히 창대하리라
Ijapokuwa mwanzo wako ulikuwa mdogo, lakini mwisho wako utakuwa wa mafanikio.
8 청컨대 너는 옛시대 사람에게 물으며 열조의 터득한 일을 배울지어다
“Ukaulize vizazi vilivyotangulia na uone baba zao walijifunza nini,
9 (우리는 어제부터 있었을 뿐이라 지식이 망매하니 세상에 있는 날이 그림자와 같으니라)
kwa kuwa sisi tumezaliwa jana tu na hatujui lolote, nazo siku zetu duniani ni kama kivuli tu.
10 그들이 네게 가르쳐 이르지 아니하겠느냐 그 마음에서 나는 말을 발하지 아니하겠느냐
Je, hawatakufundisha na kukueleza? Je, hawataleta maneno kutoka kwenye kufahamu kwao?
11 왕골이 진펄이 아니고 나겠으며 갈대가 물 없이 자라겠느냐
Je, mafunjo yaweza kumea mahali pasipo na matope? Matete yaweza kustawi bila maji?
12 이런 것은 푸르러도 아직 벨 때 되기 전에 다른 풀보다 일찌기 마르느니라
Wakati bado yanaendelea kukua kabla ya kukatwa, hunyauka haraka kuliko majani mengine.
13 하나님을 잊어버리는 자의 길은 다 이와 같고 사곡한 자의 소망은 없어지리니
Huu ndio mwisho wa watu wote wanaomsahau Mungu; vivyo hivyo matumaini ya wasiomjali Mungu huangamia.
14 그 믿는 것이 끊어지고 그 의지하는 것이 거미줄 같은즉
Lile analolitumainia huvunjika upesi; lile analolitegemea ni utando wa buibui.
15 그 집을 의지할지라도 집이 서지 못하고 굳게 잡아도 집이 보존 되지 못하리라
Huutegemea utando wake, lakini hausimami; huungʼangʼania, lakini haudumu.
16 식물이 일광을 받고 푸르러서 그 가지가 동산에 벋어가며
Yeye ni kama mti ulionyeshewa vizuri wakati wa jua, ukieneza machipukizi yake bustanini;
17 그 뿌리가 돌 무더기에 서리어서 돌 가운데로 들어 갔을지라도
huifunganisha mizizi yake kwenye lundo la mawe, na kutafuta nafasi katikati ya mawe.
18 그 곳에서 뽑히면 그 자리도 모르는 체하고 이르기를 내가 너를 보지 못하였다 하리니
Unapongʼolewa kutoka mahali pake, ndipo mahali pale huukana na kusema, ‘Mimi kamwe sikukuona.’
19 그 길의 희락은 이와 같고 그 후에 다른 것이 흙에서 나리라
Hakika uhai wake hunyauka, na kutoka udongoni mimea mingine huota.
20 하나님은 순전한 사람을 버리지 아니하시고 악한 자를 붙들어 주지 아니하신즉
“Hakika Mungu hamkatai mtu asiye na hatia, wala kuitia nguvu mikono ya mtenda mabaya.
21 웃음으로 네 입에, 즐거운 소리로 네 입술에 채우시리니
Bado atakijaza kinywa chako na kicheko, na midomo yako na kelele za shangwe.
22 너를 미워하는 자는 부끄러움을 입을 것이라 악인의 장막은 없어지리라
Adui zako watavikwa aibu, nazo hema za waovu hazitakuwepo tena.”

< 욥기 8 >