< 욥기 5 >

1 부르짖어 보아라 네게 응답할 자가 있겠느냐 거룩한 자 중에 네가 누구에게로 향하겠느냐
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 분노가 미련한 자를 죽이고 시기가 어리석은 자를 멸하느니라
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 내가 미련한 자의 뿌리 박는 것을 보고 그 집을 당장에 저주하였노라
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 그 자식들은 평안한 데서 멀리 떠나고 성문에서 눌리나 구하는 자가 없으며
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 그 추수한 것은 주린 자가 먹되 가시나무 가운데 있는 것도 빼앗으며 올무가 그의 재산을 향하여 입을 벌리느니라
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 재앙은 티끌에서 일어나는 것이 아니요 고난은 흙에서 나는 것이 아니라
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 인생은 고난을 위하여 났나니 불티가 위로 날음 같으니라
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 나 같으면 하나님께 구하고 내일을 하나님께 의탁하리라
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 하나님은 크고 측량할 수 없는 일을 행하시며 기이한 일을 셀 수 없이 행하시나니
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 비를 땅에 내리시고 물을 밭에 보내시며
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 낮은 자를 높이 드시고 슬퍼하는 자를 흥기시켜 안전한 곳에 있게 하시느니라
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 하나님은 궤휼한 자의 계교를 파하사 그 손으로 하는 일을 이루지 못하게 하시며
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 간교한 자로 자기 궤휼에 빠지게 하시며 사특한 자의 계교를 패하게 하시므로
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 그들은 낮에도 캄캄함을 만나고 대낮에도 더듬기를 밤과 같이 하느니라
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 하나님은 곤비한 자를 그들의 입의 칼에서, 강한 자의 손에서 면하게 하시나니
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 그러므로 가난한 자가 소망이 있고 불의가 스스로 입을 막느니라
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 볼지어다 하나님께 징계받는 자에게는 복이 있나니 그런즉 너는 전능자의 경책을 업신여기지 말지니라
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 하나님은 아프게 하시다가 싸매시며 상하게 하시다가 그 손으로 고치시나니
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 여섯가지 환난에서 너를 구원하시며 일곱가지 환난이라도 그 재앙이 네게 미치지 않게 하시며
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 기근 때에 죽음에서, 전쟁 때에 칼 권세에서 너를 구속하실 터인 즉
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 네가 혀의 채찍을 피하여 숨을 수가 있고 멸망이 올 때에도 두려워 아니할 것이라
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 네가 멸망과 기근을 비웃으며 들짐승을 두려워 아니할 것은
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 밭에 돌이 너와 언약을 맺겠고 들짐승이 너와 화친할 것임이라
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 네가 네 장막의 평안함을 알고 네 우리를 살펴도 잃은 것이 없을것이며
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 네 자손이 많아지며 네 후예가 땅에 풀 같을 줄을 네가 알것이라
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 네가 장수하다가 무덤에 이르리니 곡식단이 그 기한에 운반되어 올리움 같으리라
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 볼지어다 우리의 연구한 바가 이같으니 너는 듣고 네게 유익된 줄 알지니라
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< 욥기 5 >