< 욥기 40 >

1 여호와께서 또 욥에게 말씀하여 가라사대
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 변박하는 자가 전능자와 다투겠느냐 하나님과 변론하는 자는 대답할지니라
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 욥이 여호와께 대답하여 가로되
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 나는 미천하오니 무엇이라 주께 대답하리이까 손으로 내 입을 가릴 뿐이로소이다
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 내가 한두번 말하였사온즉 다시는 더하지도 아니하겠고 대답지도 아니하겠나이다
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 여호와께서 푹풍 가운데서 욥에게 말씀하여 가라사대
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 너는 대장부처럼 허리를 묶고 내가 네게 묻는 것을 대답할지니라
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 네가 내 심판을 폐하려느냐 스스로 의롭다 하려 하여 나를 불의 하다 하느냐
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 네가 하나님처럼 팔이 있느냐 하나님처럼 우렁차게 울리는 소리를 내겠느냐
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 너는 위엄과 존귀로 스스로 꾸미며 영광과 화미를 스스로 입을지니라
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 너의 넘치는 노를 쏟아서 교만한 자를 발견하여 낱낱이 낮추되
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 곧 모든 교만한 자를 발견하여 낮추며 악인을 그 처소에서 밟아서
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 그들을 함께 진토에 묻고 그 얼굴을 싸서 어둑한 곳에 둘지니라
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 그리하면 네 오른손이 너를 구원할 수 있다고 내가 인정하리라
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 이제 소 같이 풀을 먹는 하마를 볼지어다 내가 너를 지은 것같이 그것도 지었느니라
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 그 힘은 허리에 있고 그 세력은 배의 힘줄에 있고
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 그 꼬리 치는 것은 백향목이 흔들리는 것같고 그 넓적다리 힘줄은 서로 연락되었으며
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 그 뼈는 놋관 같고 그 가릿대는 철장 같으니
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 그것은 하나님의 창조물 중에 으뜸이라 그것을 지은 자가 칼을 주었고
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 모든 들 짐승의 노는 산은 그것을 위하여 식물을 내느니라
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 그것이 연 줄기 아래나 갈 밭 가운데나 못속에 엎드리니
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 연 그늘이 덮으며 시내 버들이 둘렀구나
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 하수가 창일한다 할지라도 그것이 놀라지 않고 요단강이 불어 그입에 미칠지라도 자약하니
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 그것이 정신 차리고 있을 때에 누가 능히 잡을 수 있겠으며 갈고리로 그 코를 꿸 수 있겠느냐
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< 욥기 40 >