< 욥기 38 >

1 때에 여호와께서 폭풍 가운데로서 욥에게 말씀하여 가라사대
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 무지한 말로 이치를 어둡게 하는 자가 누구냐
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 너는 대장부처럼 허리를 묶고 내가 네게 묻는 것을 대답할지니라
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 내가 땅의 기초를 놓을 때에 네가 어디 있었느냐 네가 깨달아 알았거든 말할지니라
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 누가 그 도량을 정하였었는지 누가 그 준승을 그 위에 띄웠었는지 네가 아느냐
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 그 주초는 무엇 위에 세웠으며 그 모퉁이 돌은 누가 놓았었느냐
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 그 때에 새벽 별들이 함께 노래하며 하나님의 아들들이 다 기쁘게 소리하였었느니라
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 바닷물이 태에서 나옴 같이 넘쳐 흐를 때에 문으로 그것을 막은 자가 누구냐
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 그 때에 내가 구름으로 그 의복을 만들고 흑암으로 그 강보를 만들고
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 계한을 정하여 문과 빗장을 베풀고
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 이르기를 네가 여기까지 오고 넘어가지 못하리니 네 교만한 물결이 여기 그칠지니라 하였었노라
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 네가 나던 날부터 아침을 명하였었느냐 새벽으로 그 처소를 알게 하여
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 그것으로 땅끝에 비취게 하고 악인을 그 가운데서 구축한 일이 있었느냐
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 땅이 변화하여 진흙에 인친 것 같고 만물이 옷 같이 나타나되
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 악인에게는 그 빛이 금한바 되고 그들의 높이 든 팔이 꺾이느니라
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 네가 바다 근원에 들어갔었느냐 깊은 물밑으로 걸어 다녔었느냐
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 사망의 문이 네게 나타났었느냐 사망의 그늘진 문을 네가 보았었느냐
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 땅의 넓이를 네가 측량하였었느냐 다 알거든 말할지니라
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 광명의 처소는 어느 길로 가며 흑암의 처소는 어디냐
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 네가 능히 그 지경으로 인도할 수 있느냐 그 집의 길을 아느냐
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 네가 아마 알리라 네가 그 때에 났었나니 너의 년수가 많음이니라
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 네가 눈 곳간에 들어갔었느냐 우박 창고를 보았느냐
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 내가 환난 때와 전쟁과 격투의 날을 위하여 이것을 저축하였노라
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 광명이 어느 길로 말미암아 뻗치며 동풍이 어느 길로 말미암아 땅에 흩어지느냐
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 누가 폭우를 위하여 길을 내었으며 우뢰의 번개 길을 내었으며
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 사람 없는 땅에, 사람 없는 광야에 비를 내리고
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 황무하고 공허한 토지를 축축하게 하고 연한 풀이 나게 하였느냐
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 비가 아비가 있느냐 이슬 방울은 누가 낳았느냐
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 얼음은 뉘 태에서 났느냐 공중의 서리는 누가 낳았느냐
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 물이 돌 같이 굳어지고 해면이 어느니라
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 네가 묘성을 매어 떨기 되게 하겠느냐 삼성의 띠를 풀겠느냐
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 네가 열두 궁성을 때를 따라 이끌어 내겠느냐 북두성과 그 속한 별들을 인도하겠느냐
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 네가 하늘의 법도를 아느냐 하늘로 그 권능을 땅에 베풀게 하겠느냐
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 네 소리를 구름에 올려 큰 물로 네게 덮이게 하겠느냐
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 네가 번개를 보내어 가게 하되 그것으로 네게 우리가 여기 있나 이다 하게 하겠느냐
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 가슴 속의 지혜는 누가 준 것이냐 마음 속의 총명은 누가 준 것이냐
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 누가 지혜로 구름을 계수하겠느냐 누가 하늘의 병을 쏟아
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 티끌로 진흙을 이루며 흙덩이로 서로 붙게 하겠느냐
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 네가 암사자를 위하여 식물을 사냥하겠느냐 젊은 사자의 식량을 채우겠느냐
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 그것들이 굴에 엎드리며 삼림에 누워서 기다리는 때에니라
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 까마귀 새끼가 하나님을 향하여 부르짖으며 먹을 것이 없어서 오락가락 할 때에 그것을 위하여 먹을 것을 예비하는 자가 누구냐
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< 욥기 38 >